Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, naunga mkono hoja, lakini pia naomba kumpongeza Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanayofanya. Pamoja na kazi nzuri zinazofanywa na Wizara, naomba kuchangia hoja kwa kuangazia maeneo machache kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, uhamasishaji wa akinamama kujifungulia zahanati, vituo vya afya na hospitali. Kuna changamoto kubwa ya wodi za kujifungulia, wataalam na vifaa katika facilities tulizonazo katika Wilaya ya Longido. Vijiji vingi havina zahanati na kwa vichache viliyonavyo nafasi na huduma hazitoshelezi kulingana na uhitaji.

Naomba Serikali iongeze kasi katika kujenga zahanati na vituo vya afya katika vijiji na Kata za Ketumbeine, Kimokouwa/Namanga na Tarafa ya Enduiment.

Mheshimiwa Naibu Spika, Suala la Afya kwa Umma (Public Health); Wilaya ya Longido tuna changamoto kubwa ya kutokuwa na gari la kuzoa taka kwenye miji yetu midogo na pia gari la kunyonya maji machafu vyoo vinapojaa. Naomba kumuuliza Waziri kuwa Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa watu kila wilaya (Halmashauri) imepata gari la taka na la kunyonya maji machafu kwenye vyoo hasa vya Taasisi za Umma kama hospitali, shule na kwingineko?

Mheshimiwa Naibu Spika, upatikanaji dawa kwenye zahanati na vituo vya afya; katika Wilaya ya Longido, tuna kata ambazo zinategemea zahanati moja tu kama Namanga ni kuwa Idadi ya Wakazi ni kubwa sana (zaidi ya wakazi 12,000) mgao wa dawa wanayopata kila baada ya miezi mitatu toka MSD hazimalizi hata mwezi mmoja kabla ya kwisha na wananchi hulazimika kwenda kununua madawa kwenye maduka ya binafsi. Hali hii imepelekea wananchi kutoona manufaa ya kujiunga na Mfuko wa Bima ya Jamii (CHF) kwa sababu hawapati dawa nyakati zote. Naomba kuishauri Serikali kugawa dawa kulingana na idadi ya watu na wanaohudumiwa katika kituo husika badala ya kuangalia kiwango kuwa ni zahanati au kituo cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mandatory Health Cover, ulazima wa kila mtu/Mtanzania kuwa na Bima ya Afya); naunga mkono hoja ya kutaka kila Mtanzania kuwa na Bima ya Afya, lakini nashauri kuwa kabla ya kupitisha Sheria ya kusimamia zoezi hili, Serikali ihakikishe kuwa kila kituo cha huduma ya Afya (Zahanati, Kituo cha Afya, Hospitali) kinakuwa na dawa zate za msingi wakati wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, Uhaba wa nyumba za Wahudumu wa Afya hasa vijijini; katika Wilaya ya Longido tuna changamoto kubwa ya nyumba za Wauguzi hasa katika Zahanati zetu za vijijini. Kwa mfano katika Kijiji cha Losirwa, Kata ya Iloinenito, Tarafa ya Longido, Madaktari na Nesi wanaishi ndani ya zahanati kutokana na ukosefu wa nyumba za kuishi na kijiji kilichoko katika eneo lenye mazingira magumu kwa barabara, mawasiliano na hata maji. Naomba Serikali itenge bajeti ya kusaidia maeneo kama hayo katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumalizia ujenzi wa vituo vitatu vya afya, naomba kushukuru Serikali kwa kuwa ilitutengea fedha mwaka uliopita kwa ajili ya ujenzi wa vituo viwili vya Afya – Kata ya Engiromibor shilingi milioni 400 na Kata ya Kimokouwa shilingi milioni 700. Kwa Vituo hivi viko katika hatua za umaliziaji na fedha tulizopewa zimemalizika, naomba Serikali itenge tena fedha katika bajeti hii ili tuweze kumalizia Kituo cha Engareneibor kinahitaji shilingi milioni 269 kumalizika ni Kimokouwa tunahitaji shilingi milioni 310 kumalizia.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile tuna Kituo cha Afya kipya tulichoanza kujenga kwa nguvu za wananchi katika Tarafa ya Ketumbeine, Kata ya Ketumbaine. Tumeweza kujenga hadi kupaua na sasa naomba Serikali ituunge mkono ili kumalizia kituo hicho mwaka huu wa fedha ili kianze kutoa huduma kwa wananchi wa vijiji 20 vya Tarafa ya Ketumbeine ambao kwa miaka yote wamekuwa wakifuatilia huduma za afya Longido ambavyo kwa vijiji vingine ni zaidi ya kilomita 110 kwenye barabara mbovu za vumbi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba tena kusema naunga mkono hoja.