Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu kwa kazi nzuri wanazofanya. Nashukuru kwa kuimarisha huduma ya afya ya Mama na Mtoto hali ambayo imesababisha katika Hospitali ya Temeke mwezi Machi hakuna kifo cha uzazi. Yote hayo yametokana na kuimarika kwa huduma zote za afya ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Temeke.

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo yafuatayo yazingatiwe (changamoto):-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba mashine za CT Scan kwa Hospitali za Mkoa wa Dar es Salaam, Temeke, Mwananyamala na Amana. Hospitali hizo hazina mashine za kufulia nguo, mashuka mpaka yapelekwe Muhimbili jambo ambalo linafanya kipindi fulani mashuka yanapungua hospitalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, gharama kubwa za matibabu kwa hospitali zinazopitia Wakala wa CRDB, unatakiwa ununue kadi kwa Sh.10,000 au utumie ya Wakala kwa Sh.2,000 kila unapokwenda hospitali. Mifumo ya Serikali itumike, kwani inaweza kusaidia zaidi wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, malipo ya fedha kwa maiti ni changamoto kubwa. Mtu anapofariki na deni la dawa anatakiwa kulipiwa na ndugu, unafikia wakati ndugu wanashindwa kulipia hapo viongozi tunashirikishwa na maiti kukaa muda mrefu. Naomba Serikali watoe ufafanuzi kuhusiana na jambo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, unapoenda na mgonjwa mara nyingine Emergeny Muhimbili unamlipia mgonjwa, tena unapewa bill ya dawa usiku Sh.500,000 na zaidi, lakini baada ya sekunde unakuta mgonjwa amefariki. Kutokana na panic unaacha kila kitu, kwa nini tusiwe na kianzio cha dawa kwa wagonjwa wanaokuja kuanza matibabu kabla ya kupewa bill?

Mheshimiwa Naibu Spika, hospitali/zahanati ya Mbagala Zakhem imezidiwa sana, eneo ni dogo na wananchi wanaohitaji huduma ni wengi sana kutokana na kukua kwa Mji wa Mbagala na ongezeko kubwa la watu. Pamoja na jitihada za halmashauri kujenga zahanati ya Maji Matitu na Charambe, lakini jiografia inakataa kwa kuwa mgonjwa akitoka Zakhem anaenda Temeke na Zakhem ni katikati ya Mji wa Mbagala. Naomba Serikali isadie hata kujenga ghorofa la OPD kwa wagonjwa wa kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.