Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuipongeza Serikali yetu ya Awamu ya Tano chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa jitihada zake za kuboresha huduma ya afya kote nchini hususan ujenzi wa miundombinu ya majengo nchini kote; kupunguza upungufu mkubwa wa dawa na vifaatiba kote nchini; kupunguza upungufu mkubwa wa watumishi wa kada za afya kote nchini; kupambana na maambukizi ya VVU nchini na mpango mkakati wake wa kuboresha sekta hii kila mwaka, hali inayowafanya wananchi kuwa na imani kubwa kwa Serikali yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara itazame upya mtawanyiko wa Madaktari katika Hospitali za Wilaya na Mikoa ili kuhakikisha angalau kila hospitali inapata mtaalam mmoja kwa kila kitengo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali iangalie sera ya familia kutunza wazee na watoto kupitia familia zao badala ya kutelekeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, maombi ya Hospitali ya Mji wa Mbulu kupatiwa gari la kusafirisha wagonjwa (ambulance) kwani gari lililoko limechakaa sana na wagonjwa wengi wanapata rufaa ya kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Haydom na KCMC Moshi nako ni mbali sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi la Tarafa ya Nambis katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu haina hata kituo kimoja katika kata zote tano na ni mbali kutoka Hospitali ya Wilaya hali inayosababisha akinamama wajawazito kukosa huduma na kutembea zaidi ya kilomita 30 mpaka 40 kufika Mbulu Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naomba Mheshimiwa Waziri wa Afya afanye ziara katika Jimbo la Mbulu Mjini hususan Tarafa hiyo ya Nambis kwa kuwa alishaahidi kufanya ziara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.