Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji mzuri sana na nimtakie mfungo mtukufu wa Ramadhani (Ramadhan Kareem).

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishukuru sana Serikali kwa kutuboreshea Kituo cha Afya cha Malya, kwa niaba ya wananchi wanaozunguka kituo hicho pamoja na wa Jimbo la Maswa, tunaomba kutupatia watalaam hasa daktari, aliyepo ni clinical officer, Wauguzi na wahudumu pamoja na watalaam wa maabara, Wafamasia na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumkumbusha Mheshimiwa Waziri ombi la gari kwa ajili ya hospitali ya Sumve kama barua yetu kwako tuliyowasilisha kutokana na jiografia ya eneo. Gari hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa sana kuokoa maisha ya wazazi na watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitangulize ombi la kukiboresha Kituo cha Afya cha Nyambiti. Nyambiti ni Mji unaokuwa kwa kasi na kwa haraka sana kutokana na kuwa na viwanda viwili vya kuchambua pamba. Kuna kituo cha treni (railway station), sekondari mbili, shule za msingi nne na jamii inayoendelea kukua. Naomba katika mpango wa uboreshaji wa vituo vya afya, Kituo cha Afya cha Nyambiti kiwe kimojawapo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimtakie Mheshimiwa Waziri Ummy kila la kheri katika njozi zake na Mungu atamsimamia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono.