Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mansoor Shanif Jamal

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MANSOOR S. HIRAN: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kazi nzuri ambayo anafanya na wasaidizi wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue nafasi hii kushukuru kwa kutuletea ambulance mpya kwa ajili ya Kituo cha Mwamashimba.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Kwimba ambayo iko Ngudu ina changamoto nyingi; hatuna mashine ya kufua nguo, x-ray ni ya zamani sana inaharibika mara kwa mara, ni analogue, tunaomba digital, duka la dawa la MSD, tunaomba watufungulie pale kwenye hospitali yetu ili wananchi wapate dawa kwa bei nafuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Daktari wa Macho walituletea lakini sehemu ya kufanyia kazi hakuna, hatuna chumba cha huduma ya macho, tuna jengo, lakini halijakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri watoto wetu wanaokwenda shule za msingi na sekondari wengi wana magonjwa yafuatayo; pumu, sikosell, kisukari. Watoto wengi wanapata shida shuleni lakini Mwalimu hana uwezo wa kuwasaidia kwa sababu hatujawawezesha. Nashauri Mheshimiwa Waziri awapatie emergency kit kwenye shule zote za msingi na sekondari na Walimu wafundishwe jinsi ya kutoa first aid kwa mtoto ili wakati anapelekwa hospitali awe amepata huduma ya kwanza ili maisha yake yapone.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Hungumarwa unakua kwa kasi kubwa sana, tunaomba watujengee kituo cha afya kwani zahanati zinaelemewa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.