Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa Serikali kwa ujumla na kwa Wizara kwa namna ya pekee kwa kazi nzuri. Changamoto za Wizara hii (Sekta ya Afya) ni nyingi na za muda mrefu na za aina mbalimbali, hivyo, hata utatuzi wake unahitaji muda, rasilimali fedha na kadhalika, lakini taratibu zitapungua sana kutokana na kasi hii. Nawatakikakila la kheri.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto Kitaifa, ziko nyingi bado, lakini hotuba ya Waziri Ukarasa 155 wa kitabu cha hotuba umeainisha vipaumbele vya Wizara na Bajeti kwa mwaka huu. Wakipata fedha kila mwaka, kama wanavyoomba watafanikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika vipaumbele 11, nimechagua kipaumbele cha (iii) na cha (v) ambavyo vinagusa pia moja kwa moja Jimbo la Tunduru Kaskazini na Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Wataalam; uhaba wa Wataalam Kitaifa ni 50% na Tunduru ni 35%. Serikali iendelee kuzalisha Wataalam kupitia Vyuo vyetu vilivyopo, Mabaraza ya Wanataaluma na Bodi za Ushauri yafanye kazi zao vema, ikiwa ni pamoja na kusimamia Professional Ethics, Kanuni za Kusimamia Taaluma ikiwemo mafunzo ya utarajali zikamilike na zitumike, pia (CPD - Continuing Professional Development) iwekewe msisitizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua za kushughulikia nidhamu ya Wataalam zitokane na Vyombo vya Taaluma, isipokuwa kwa makosa yasiyokuwa na kitaalam, watumishi waboreshewe maslahi yao, Vyuo viongoze udahili, uwiano (Ratio) kati ya Madaktari na Wataalamu wa Kada nyingine za juu na Wataalam wa Kada za Kati kwa mujibu wa ILO uzingatiwe. Hatua hii itatoa nafasi ya utoaji wa huduma bora, concentration na kupumzika vikiwa ni vichocheo vinavyotegemeana.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru na Jimbo la Tunduru Kaskazini; Hospitali ya Wilaya ni ya siku nyingi, imechakaa (miundombinu), tunaomba ifanyiwe ukarabati. Chumba cha upasuaji mkubwa (major theatre), chumba cha upasuaji mdogo, (minor theatre) OPD, X –Ray, RCH, Maabara, Wards miundombinu yote hii ni chakavu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vifaa tiba; Vituo vya Afya na Zahanati; Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Jimbo la Tunduru Kaskazini lina Kata 24, lakini kuna Vituo vya Afya viwili na kimoja ambacho kinajengwa. Tunaomba Ambulance ziweze kusaidia kutoa huduma kwa Vituo vya Afya viwili ambavyo viko kilomita 64 pande tofauti (1800).

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Kituo cha Afya cha Nakapanya kipatiwe fedha kwa ajili ya ukarabati kama tulivyobahatika kwa Kituo cha Matemanga. Hii inachagizwa na ukweli huu wa idadi ndogo ya Vituo vya Afya, vitatu tu katika Kata 24. Zahanati pia ni chache, lakini kwa sasa tukiboreshewa Vituo vya Afya tulivyonavyo kwa Wataalam, miundombinu na Vifaa tiba na kupatiwa Ambulances itatusaidia sana.