Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuwapongeza Viongozi wa Wizara hii, Waziri Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile kwa kazi nzuri wanayofanya ya kusimamia Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu utajikita katika maeneo matatu. Kwanza, Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini inayojengwa Mtwara. Ujenzi wa Hospitali hii umeanza muda mrefu na sasa umesimama. Mheshimiwa Waziri alipotembelea ujenzi huu mwaka juzi aliahidi kuwa ni bora jengo lililopo likakamilika na baadhi ya Idara zikaanza kufanya kazi. Nashauri ujenzi uendelezwe kwenye eneo hili na hospitali ifunguliwe kwa kuanza na idara ambazo zinaweza kutumia jengo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mtwara (Ligula). Hospitali hii inahitaji ukarabati mkubwa wa majengo yake na ina idadi chache ya watumishi kwa maana ya madaktari na wauguzi. Hatua zichukuliwe ili kukabiliana na changamoto hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, dawa za magonjwa yasiyoambukiza (kisukari na shinikizo la juu la damu). Kuna ongezeko kubwa la wagonjwa wa magonjwa hayo na kwa kuwa wagonjwa hao hutumia dawa muda mrefu na bei zake ni za juu, nashauri Serikali iangalie kwa karibu tatizo hili kwa kufanya yafuatayo:-

(i) Kuwa na programu za kutoa elimu kwa jamii ili kupunguza watu wanaoambukizwa;

(ii) Kuhakikisha kuwa dawa zinapatikana kwa bei nafuu hadi ngazi za chini; na

(iii) Kliniki za binafsi zidhibitiwe kwa kuwa zinatoa huduma kwa bei ya juu.