Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Wakurugenzi na wafanyakazi wote wa Wizara hii kwa kazi kubwa wanayoifanya. Hakika mnaitendea haki Wizara hii, nawatakia kila la kheri.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru sana kutembelewa na Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu kwa nyakati tofauti. Ziara zote zimezaa matunda ya msaada wa kifedha na vifaa, ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wilaya ya Urambo ina vijiji 59, zahanati 22, tunaomba tusaidiwe kumalizia maboma 8 ambayo yamejengwa ili tuongeze huduma kwa wananchi. Tuna kata 18, vituo vya afya vipo viwili, kimoja kimekamilika tunashukuru na kimoja kinaendelea kujengwa. Tunaomba tuongezewe vituo viwili katika Kata za Songambele na Vumilia ambapo wananchi wameanza msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Kituo cha Afya Uyogo ambacho wananchi wanajenga kwa kushirikiana na marafiki kutoka Uingereza. Tunaomba ahadi za Waziri zitimizwe za ambulance kwa kuwa ni mbali na Hospitali ya Wilaya na tupewe shilingi milioni 20 alizoahidi ili kukamilisha kituo kinachojengwa. Vilevile, tunaomba tupewe shilingi milioni 50 alizoahidi Waziri alipotembelea Kituo cha Afya cha Usoke kwa lengo la kukamilisha miundombinu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kupitia mradi wa ADB ulianza kujenga jengo la theater ambalo liko tangu mwaka 2010. Tunaomba Serikali itusaidie kumalizia jengo hilo ambalo linahitaji fedha zipatazo shilingi milioni 200.

Mheshimiwa Naibu Spika, Urambo haina chumba cha wagonjwa mahututi (ICU). Kuna jengo lililoanza kujengwa kwa mpango wa LGDG linaloweza kukamilika kwa gharama ya shilingi milioni 20. Tunaomba Waziri akumbuke ahadi hii na aitekeleze.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Mheshimiwa Waziri aliahidi kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ya kukamilisha wodi ya akina mama. Tunaomba tusaidiwe fedha hizo kwa ajili ya Zahanati ya Itebulanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Urambo ina X- ray ya kizamani ya analogue. Tunaomba X-ray ya kisasa ya digital.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, tunaomba tuongezewe wafanyakazi kwa kuwa tuna upungufu wa asilimia 48.