Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, maombi ya vifaa vya upasuaji. Naishukuru Wizara kwa kuelewa hali halisi ya Hospitali ya Mafinga ambayo inahudumia Halmashauri ya Mafinga Mji, Mufindi DC na Wilaya za jirani ikiwemo Mbarali (Madibira), Mlimba, Iringa Vijijini na Makambako na hivyo Serikali kutupatia fedha za kujenga na kuboresha Kituo cha Afya cha Ihongole angalau imeleta nafuu kwa Hospitali ya Mafinga ambayo pia ipo kandokando ya barabara kuu ya Tanzania-Zambia (TANZAM I).

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na huduma kuendelea kuboreshwa, tumejikuta idadi ya watu wanaohudumiwa ikiongezeka hasa akina mama wajawazito ambao theluthi moja hufanyiwa upasuaji. Kutokana na hali hiyo, tulipata msaada kutoka Ubalozi wa Japan ambapo tumejenga jengo la upasuaji. Hata hivyo, msaada huo ulihusu jengo tu na siyo vifaa. Halmashauri tumejipanga na tumenunua baadhi ya vifaa. Naomba Wizara ione uwezekano wa kutusaidia baadhi ya vifaa ili tufungue na tuanze kutoa huduma kwa baadhi ya vyumba kwa kuwa jengo lina vyumba vitatu vya upasuaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mchango huu wa maandishi, naambatanisha barua ambayo niliwasilisha kwako na maelezo ya ziada kuhusu mradi huu. Naamini chochote kitu, anything can make a difference. Nafahamu mna jukumu kubwa kupitia MSD, tunaomba sehemu ya vifaa tusaidiwe kwa kiwango chochote.