Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, nitangulie kwa kuunga mkono hoja hii ya Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Naibu wake, Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, bila kumsahau Katibu Mkuu wa Wizara hii, Mheshimiwa Dkt. Zainab Chaula kwa kazi nzuri wanayoifanya katika nchi hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizi, naomba kukukumbushia ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto alipokuja Itigi katika Hospitali ya Rufaa ya St.Gaspar katika Siku ya Wauguzi 2017 na kuahidi kutoa gari kwa Kituo cha Afya Mitundu ambacho kipo zaidi ya kilometa 100 toka Hospitali yetu ya Wilaya ya Manyoni. Nia yangu ni kukukumbusha tu ahadi hii aliyoitoa kwa wananchi wa Halmashauri ya Itigi, Jimbo la Manyoni Magharibi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nirudie kuunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja, ahsante.