Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Moshi. Manispaa ya Moshi ina mahitaji makubwa sana ya Hospitali ya Wilaya kwa vile Hospitali ya Mkoa ya Mawenzi imezidiwa na wagonjwa na Hospitali ya KCMC pia imezidiwa na wagonjwa. Hospitali zote hizi mbili zinahudumia wagonjwa kutoka maeneo mbalimbali nje ya Manispaa ya Moshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Manispaa ya Moshi ina eneo ambalo imelitenga kwa ajili ya ujenzi huo wa Hospitali ya Wilaya. Hivyo, ni matumaini yangu kwamba Serikali italifanyia kazi ombi langu kwa niaba ya wananchi wa Moshi Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupandishwa hadhi vituo vitatu vya zahanati kuwa vituo vya afya. Manispaa ya Moshi imeleta maombi ya muda mrefu Serikalini ya kupandisha hadhi zahanati tatu za Shirimatunda, Msaranga na Longuo B. Maombi hayo ni muhimu sana kwa vile idadi ya watu inaongezeka kila siku katika Manispaa ya Moshi. Kutokana na ongezeko hilo, mahitaji ya huduma ya matibabu yanaongezeka kwa kasi. Naomba Serikali ipandishe hadhi zahanati tajwa hapo juu kuwa vituo vya afya ili kuwasaidia wananchi kupata huduma kirahisi zaidi na kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa niaba ya wananchi wa Manispaa ya Moshi, Serikali itenge fedha kwa ajili ya kuboresha kituo cha afya kimoja katika Manispaa ya Moshi ili kutoa huduma bora kwa wakazi wa Manispaa ya Moshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.