Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, napenda kuwapongeza Waziri na Naibu wake kwa kazi kubwa wanayoifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Handeni Mji ni ya zamani na kwa sasa inaelemewa sana na idadi ya wagonjwa. Inahudumia majimbo almost manne na mpaka sasa hakuna utaratibu wa kupata hospitali katika majimbo haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu, tuna zahanati eneo la Kwamagome ambalo Mheshimiwa Waziri Ummy alifika kwenye ufunguzi, tumefikia pazuri na ikiwezekana tunaweza kupafanya pale na kuwa kituo cha afya. Naomba Waziri aliangalie eneo hili ili kuondoa msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, kule kwetu hatujapata mgao wowote kwenye kuongeza au kujenga kituo cha afya. Tunaomba Wizara itufikirie na sisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.