Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mansoor Shanif Jamal

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MANSOOR S. HIRAN: Mheshimiwa Mheshimiwa, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami nichangie hoja ambayo iko mbele yetu. Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa pumzi nami nipate nafasi ya kusimama hapa na kuzungumza ndani ya Bunge hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii pia kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara ya Afya kwa kazi nzuri ambayo wanafanya. Naomba kwanza kabisa nichukue nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kutupatia ambulace ambayo ilikuwa ni shida kubwa kwenye Kituo chetu cha Afya cha Mwamashimba. Ilikuwa ni ahadi yangu wakati wa kampeni na nashukuru sana amenisaidia ambulance mpya, ambayo nimetimiza ahadi ya wananchi wangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Kwimba Makao Makuu yetu ni Wilaya ya Ngudu Mjini. Ngudu Mjini tuna Kituo cha Afya ambacho tunakitumia kama Hospitali ya Wilaya. Kituo cha Afya hiki kina changamoto nyingi. Naomba niseme baadhi ya changamoto ambazo tunazo. Kwanza, hatuna mashine ya kufua nguo. Hospitali ile ni kubwa, inatoa huduma kwa wagonjwa wengi, kuna magonjwa ya kuambukiza, unakuta shuka zile zote zinaoshwa na binadamu ambaye anaweza akapata magonjwa, anapata shida sana kuosha hizo shuka. Kwa hiyo, namwoamba sana Mheshimiwa Waziri mashine ya kufulia nguo ili Hospitali yetu iweze kutoa huduma inayostahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto nyingine tuliyonayo ni kwamba kuna extra machine ambayo ni analogy, tuliletewa zaidi ya miaka 15, tuna X-Ray machine ya zamani sana ambayo kwa kweli inaharibika mara kwa mara. Tunaomba sana tuletewe X-Ray machine ya digital kwa sababu huduma ya X-Ray machine ni kubwa sana kwa sababu ile ina Majimbo mawili, tuna changamoto ya wagonjwa wengi sana na X-Ray inapatikana pale Wilaya ya Ngudu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ningependa kusema tatizo tulilonalo kwenye Hospitali yetu ya Wilaya ni kwamba tuliletewa Daktari wa macho, miaka miwili yuko pale, lakini hana vifaa vya kufanya kazi, hana chumba cha kufanyia kazi. Kwa hiyo, amekaa pale, anaangalia, anatoa huduma pale huku amekaa nje. Naiomba Wizara itutengenezee chumba, itupe vifaa ili huyo Daktari atoe huduma ya macho kwa wananchi wa Wilaya ya Kwimba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine tunaomba tupate pharmacy ya duka la MSD la dawa. Dawa ni shida, zinapatikana mitaani kwa bei kubwa sana, naomba MSD wafungue duka la dawa kwenye Hospitali yetu ya Wilaya angalau wananchi wapate huduma ya kununua dawa kwa bei nafuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ningependa kusema ni kwamba sisi mji wetu wa Hungumarwa unakuwa kwa kasi kubwa sana, tuna Zahanati pale ambayo inatoa huduma sawa na Kituo cha Afya. Tunaomba sana tujengewe Kituo cha Afya kwenye Kata yetu ya Hongumarwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine napenda kusema ambacho kinanipa shida sana, Mheshimiwa Waziri anisikie kwa usikivu kidogo ni kwamba watoto wetu shuleni wanapata shida. Wengi wanapoteza maisha yao kwa sababu wanaugua. Kuna magongwa matatu ambayo watoto wanapata mara kwa mara; ugonwa wa pumu, Sickle cell na Kisukari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwa Wizara, tungeweza kupata First Aid Kit ambazo tungezipeleka kwenye shule zetu zote za msingi na sekondari na pia walimu tukawafundisha ili waweze kutoa First Aid. Mara nyingi tunakuta unapoteza watoto kwa sababu shuleni wanapougua mwalimu anachofanya ni kumpeleka mtoto nyumbani badala ya kumpa First Aid na kumpeleka Hospitalini, anampeleka nyumbani unakuta mtoto anapoteza maisha yake, kitu ambacho tungeweza kuepusha, mtoto akapata First Aid shuleni ili akifika hospitalini anakuwa ameshapata First Aid.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina mengi ya kusema, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)