Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru kwa kunipa nafasi hii leo tarehe 6 Mei. Pia namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kufika katika Bunge hili na afya tele. Tatu natoa pole kwa mfanyabiashara Dkt. Reginald Mengi Mungu amuweke mahala pema peponi huyu Mheshimiwa miaka ya 80 huko tulimuita Kilwa akawa mgeni rasmi ni katika kuchangia elimu Wilaya ya Kilwa alitoa shilingi milioni 20, enzi hizo milioni 20 nyingi sana, kwa hiyo, tunatoa pole za dhati watu wa Kilwa na Ishallah Mwenyezi Mungu amuweke mahali anapostahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu 1961 tunapata uhuru mpaka leo miaka 58 Bunge linazungumzia habari ya maji, kila Mbunge anayesimama hapa anasema kwake hakuna maji sio Mbunge wa CCM wala sio Mbunge wa CUF, wala wa CHADEMA. Naomba sana ombi langu kubwa sana katika mfuko wa maji tuongeze shilingi 50 ili yapatikane maji, naona tatizo kubwa ni fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Waziri shilingi 50 iongezwe katika mfuko wa maji ili watu tupate maji. Waheshimiwa maji ndio maisha bila maji kila kitu hakifanayiki kwa hiyo, naomba mheshimiwa Waziri tunawasaidia wafadhili kwamba tutoe shilingi 50 tuingoze katika mfuko wa maji tafadhali, hilo jambo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili sisi Kilwa kuna miradi ya DCA miradi 17 lakini mpaka sasa hivi vimechimbwa visima vitatu tu tunaipongeza Serikali kwa mfano hivyo visima vitatu vyote vimechimbwa katika Jimbo langu. Lakini katika visima vitatu kisima ambacho kina maji safi na salama ni kisima kimoja tu cha Pande lakini kule Kisongo na Limaliyao visima vyote viwili maji yake ya chumvi na tulisema siku nyingi sana kwamba mazingira ya Limaliyao na Pande tunapenda tuletewe mabwawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulisema kwamba kule mazingira yake ukichimba maji lazima yawe maji ya chumvi, tunaipongeza sana Serikali Limaliyao wamechimba visima si chini ya sita lakini vyote ni maji ya chumvi. Kwa hiyo, tunaiomba Serikali mabwawa yajengwe katika maeneo hayo ya Limaliyao tunaiomba sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili tunashukuru hiki kisima cha Pande kina maji mengi na mazuri hakina mataatizo kabisa kwa saa moja inatoa lita 14,000. Kwa hiyo, tunachoomba sasa miundombinu yanaweza yakapelekwa maji katika vijiji vitatu katika eneo hilo kwa hiyo tunamuomba Mheshimiwa Waziri Ustadhi Mheshimiwa Profesa Mbarawa onesha ujasiri wako ili tupate maji katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tumepata hela tumeona katika kitabu tumepata hela milioni 300 kwa ajili ya Mji wa mdogo wa Masoko. Lakini Mheshimiwa Profesa kuna Mji mdogo wa Kivinje hakuna bajeti katika mradi wowote wa maji katika Mji mdogo wa Kivinje na Mji mdogo wa Kivinje kuna hospitali ya Wilaya na siku nyingi nasema hiyo hospitali ya Wilaya ina upungufu mkubwa wa maji. Naomba sana Mheshimiwa Profesa uangalieni Mji wa Kivinje ambao una wakati si chini watu 15,000 lakini maji hamna kabisa na hakuna mpango wowote wa maji niliouna katika kitabu hiki ambapo umepangwa mji mdogo wa Kilwa Kivinje isipokuwa Mji wa Kilwa Masoko Alhamdulillah maji yapo na kuna mradi vile vile unakwenda huko, lakini tunaomba sana Mji wa Kilwa Kivinje upatikane maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo kuna vijiji havina maji machache sana kwa mfano Kata ya Kikole kuna Luwate, kuna Kikole yenyewe, kuna kijiji cha Kisange mbalambala , maji nayo hakuna. Pia kata ya Likawage kuna kijiji kimoja kinaitwa Nainokwe kilikuwa katika mradi wa visima 10 kisima kimechimbwa hakina maji hata kidogo tunaomba nacho kijiji hiko kipatiwe maji, naomba sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kijiji cha Mavuji, kijiji cha Mchakama, Kijiji cha Mkondaji katika Kata ya Mandawa navyo maji hakuna lakini nasisitiza sana kuna mradi wa Mavuji ambao mradi huo ulikuwa chini ya Wabeligiji lakini ikaonekana hela ziko nyingi sana, sasa hivi umeingia katika mpango wa msaada wa India.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Profesa sana tena sana mradi huo wa Mavuji kama hautafanikiwa matatizo ya maji katika Mji mdogo wa Kivinje, Mji mdogo wa Masoko utamalizika nakuomba sana na kwa kuwa Serikali hii ni sikivu Serikali hii ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli ni sikivu naamini kabisa kwamba mradi huu wa Mavuji huu tutafanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabisa Mheshimiwa Dkt. Magufuli sikivu kuna mradi wangu mmoja wa barabara kwa Nkocho Kivinje paka nikaitwa mimi jina langu Nkocho kwa Kivinje, nikamuomba siku moja tu sasa hivi lami ilishakwisha iko moto imekwisha lami, ilishajengwa ni sikivu Mheshimiwa Dkt. Magufuli ni msikivu. Lakini msimuangushe nakuombe Mheshimiwa Prof. Mbarawa usimuangushe hebu fanya mpango wa maji yawe safi haya ili Mheshimiwa Dkt. Magufuli apate sifa yake hiyo inayotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hayo namuomba Mheshimiwa Magufuli kila kizuri kidogo kutakuwa na kasoro kidogo hawa watu wanaotekwa aseme na yeye kauli aseme kina Mdude hawa nao kukaa kwake kimya kuna…

MWENYEKITI: wewe ongelea hoja iliyo mbele yako tu hapa wewe na muda wako.

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, basi naendelea na maji.

MWENYEKITI: Muda wako ndio huo unga mkono upate maji, Mheshimiwa Bungara unga mkono jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli upate maji.

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya Kambi naunga mkono.