Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa dakika tano na mimi niseme kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, Prof. Mbarawa ulikuwa na Mheshimiwa Rais pale Nyamongo na nafikiri ndiyo agizo kubwa nchi hii ukipewa na Rais sidhani kama kuna agizo jingine unategemea kusikiliza. Rais alisema maji kwa sababu watu wa Nyamongo madini yanatoka pale yanachangia pesa nyingi kwenye pato la Taifa, ni aibu watu wale kuendelea kunywa maji ya sumu au ya visima vya kuchimba kwa majembe na Mto Mara na Ziwa Victoria lipo pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunajadili maji kwenye Mkoa wa Mara, Mkoa wa Mwanza na Mkoa wa Kagera ambako kuna ziwa linatoa maji yanaenda huko mbali na watu wanapata maji, ni mambo ambayo hayaeleweki kweli kweli kwa wananchi. Kwa hiyo, mimi nafikiri Profesa tuna watu 42,000 pale Nyamongo wanahitaji maji. Mji ule kutokuwa na maji, mji mdogo kama ule mkubwa vile ulivyokuwa na una watu, population yake 42,000 ni sawasawa na Majimbo mengi tu ya watu ambao wapo humu, hauna maji mpaka leo sielewi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili; wote tumekubaliana tatizo la maji ni kubwa kwenye nchi hii lakini tunatofautiana kwenye sehemu ndogo tu kwamba tatizo ambalo linatukumba ni priorities. Tunapangaje vipaumbele vyetu na sisi Wabunge tunasimamiaje Serikali kwenye kutekeleza hivyo vipaumbele. Sasa leo kila Mbunge anasimama humu na ni kwa mara ya kwanza naona Wabunge wanashabikia kwenda kuwawekea wananchi maskini mzigo eti tozo za shilingi 50, inanishangaza sana. sielewi kwamba leo solution kwa sababu hatuna walimu, hatuna barabara, madawati, choo hatuna kwenye shule sijui nini tuweke tozo shilingi 50, hayo mafuta si yatafika 4,000 na nani atasafiri kwenye hayo magari kama mafuta yakifika shilingi 4,000. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachosema Serikali lazima ije na mpango kwanza zile pesa tulizotenga zenyewe kwenye bajeti kwa nini hazijaenda, kwa nini hazikwenda? Je, na tozo hizo mnazozungumza tumeweka kwenye REA zimekwenda shilingi ngapi kwenye hiyo tozo ya REA? Kwa sababu pia usimamiaji wa bajeti, je tunasimamia na tunatekeleza bajeti kama tulivyozipanga hapa au sisi Wabunge tumekuja tunapiga kelele humu baadaye wanaenda wanakaa kikundi cha watu 4/5 wanatengua kila kitu ambacho Wabunge walipitisha hapa halafu mnataka tuje hapa tupige makofi eti shilingi 5; mimi hata senti moja kuongeza kwenye mafuta napinga na napinga kwa sababu inakwenda kuongezea wananchi maskini mzigo... (Makofi)

T A A R I F A

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru huyu mganga wa meno anajifunza bado Bunge linavyofanya kazi, kwa hiyo, sina haja ya kumjibu. Hapa tunazungumza mambo ya wananchi kwamba watu wana matatizo ya maji na tutoe solution kwamba Wabunge tusikwepe majukumu ya kuisimamia Serikali itoe pesa, kwa sababu wananchi hawapo humu ndiyo wanyonge wenu mnataka leo muwapelekee mzigo; kila mtu anayesimama hapa weka shilingi 50, tukija hapa hiyo shilingi 50 haijaenda nani atasimama humu aseme shilingi 50 haikwenda? Kama mna uwezo huo mbona pesa za REA hazijaenda na hampigi kelele hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi nasema Wabunge…

T A A R I F A

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hao wenzetu bado wanataka kuaminika, kwa hiyo endeleeni mtaaminika tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachosema, hoja ya maji wote tunaunga mkono lakini hoja yangu ni kwamba Wabunge wajibu wetu ni kuisimamia Serikali, amezungumza vizuri sana hapa mama Mheshimiwa Conchesta, amesema haya mambo ya kuja hapa tuna-beg naomba tumekuwa Matonya humu na vikombe, naomba piga magoti, hapana lazima Serikali ijue Wabunge wanapozungumza hapa wanawawakilisha walipa kodi wa nchi hii ambao wamejikamua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo tunasema hapa tuongeze shilingi 50 kwenye mafuta ya taa kweli? Hivi ninyi mnajua vijijini wananchi wanaoishi kijijini ambaye kutoa shilingi 2,000 ni tatizo kweli kweli na kama mna uchungu kiasi hicho, nani ame-volunteer mshahara wake humu, mnalipwa mamilioni; anzeni nyie kwamba tukatwe milioni moja moja kila mwezi iende kwenye maji kama kweli mna uchungu kiasi hicho... (Makofi)

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Acha ufisadi kwanza wa madini wewe…

MHE. JOHN W. HECHE: Hatuwezi kukubali tuje kubana wananchi wanyonge eti ndiyo wanyonge wetu kwa sababu hawapo humu, tunakwepa majukumu shilingi 50. Na hiyo itakuwa siasa ambayo tutaizungumza kwa wananchi, muelewe kabisa, shukrani. (Makofi)