Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kukushukuru sana, lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Maji kwa kuja kwangu tarehe 18 Oktoba,2018 kujionea adha ya maji ambayo ipo kwenye Jimbo langu la Tandahimba. Mheshimiwa Waziri alivyofika nadhani ameona kwa machoyake, lakini kwenye mpango huu wa maji Tandahimba tunazungumza sana Mradi wa Maji wa Makonde ambao utahudumia Wilaya ya Newala, Tandahimba na Nanyamba. Shida yangu kwenye huu mradi wanaosema waKitaifa, tulipoingia Bungeni 2016/2017, kwenye kabrasha la kitabu cha bajeti ya maji, ukisoma ukurasa ule wa 78 umezungumzwa Mradi huu wa Makonde tukiwa tunatarajia fedha za mkopo kutoka Benki ya India. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulivyorudi Bungeni 2017/ 2018, tumekuja tena kwenye ukurasa wa 80, tumeuzungumzia tena Mradi wa Maji wa Makonde tukiwa tunasubiri fedha kutoka kwenye fedha ya mkopo kutoka India. Tumekuja kwenye bajeti iliyofuata 2018/2019, ukurasa wa 64,Mradi huo wa Maji wa Makonde tunaozungumza, tunazungumzia fedha za kutoka kwa wafadhili. Tumekuja kwenye bajeti hii ya leo hii tunayoisema ya 2019/2020 ambayo inawezekana kwa sisi wengine ikawa bajeti ya mwisho tunazungumzia fedha ambazo wanataka kukopa tenasijui wapi, are we really serious tunataka mradi huu uendelee?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ajaribu kuangalia kila tukija kwenye bajeti fedha za Mradi huu wa Makonde tunazungumzia fedha za kutoka kwa wafadhili, kwa miaka minne mfululizo, hizo fedha za wafadhili hakuna, hazitoki, hawa watu kweli watapewa maji? Hebu niwaulize ndugu zangu Serikali ya Chama cha Mapinduzi wanayosema Serikali ya wanyonge,ni mnyonge gani kama mwananchi hapati maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maji ndiyo bidhaa pekee ambayo wangekuwa wanawapa Watanzania shukurani yake ingekuwa ni kubwa kuliko kitu chochote kile. Leo zinatengwa fedha mabilioni zinakwenda kwenye Stiegler’sGorge ambao watumiaji wake si wote, fedha zinakwenda kwenye reli watumiaji wake sio wote, fedha zinakwenda kwenye bombardierwapandaji wa bombardier sio wote, waweke fedha kwenye miradi ya maji ambayo itawagusa Watanzania wote. Huu ndio ukomo wa huruma kwa Serikali ya CCM kwa Watanzania. Niwaambie kabisa, kama tunataka kupima ukomo wa huruma kwa Watanzania. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia alichokisema, lakini nimkumbushe hata wakati tunazungumza Mradi waGesi ya Mtwara tulisema ndio itakuwa mwisho wa tatizo la umeme Tanzania. Leo bado tunalia na umeme, kwa hiyo sitaki kuipokea taarifa yake ile akakae nayo kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Taifa la Tanzania ambalo hatuna shida ya maji yenyewe, tuna Ziwa Victoria, kwangu Mtwara tuna Mto Ruvuma, tuna Ziwa Malagalasi amezungumza Mheshimiwa Hasna pale, tuna Ziwa Tanganyika, tuna kila vyanzo vya maji ukienda Kilimanjaro kuna maporomoko yanamwaga maji, miaka 59 toka tumepata uhuru tunarudi Bungeni tunazungumza tatizo la maji kweli miaka 59 ya uhuru!(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,niombe sana, alizungumza hapa Mzee Mheshimiwa Chenge kwamba tunayoyaazimia Bungeni basi tuyasimamie, ile Sh.50 iliyozungumzwa, niombe Jumatatu Waheshimiwa Wabunge wote kwa tatizo la maji namna lilivyo, tusimamie kuona ile 50 inaongezwa ili watu wapate maji. Watu wamezungumza vyanzo vingi tu hapa, ukienda leo watumiaji wa simu bando tu, ukichukua fedha za kwenye bando ni matrilioni ya fedha, kwa nini tusichukue fedha tukapeleka kwenye maji?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,kwenye Mradi wangu mdogo ule waMkwiti, leo nimshukuru sana ameupa fedha, lakini ule mradi una lots tatu, lot ya kwanza ndio hii ambayo amepeleka fedha ya kutoa maji kule kwenye Mto Ngwele ambako pana tanki moja. Lot ya pili utatoa Mto Ngwele kupeleka Mangombyanalot ya tatu inatoka Mangombya kupeleka vijijini, lakini fedha iliyopata ni ya lot moja. Sasa ukiangalia hii lot moja maana yake tutakaa miaka tisa ndio kukamilishe lot tatu watu wapate maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kamatuna lots tatu na fedha ikawa ipo ni bora wakaunganisha fedha wakawapa wakandarasi tofauti ili watu waone social impact ya maji ambayo wanafanya. Leo tutawaambia tuna Mradi waMaji wa Mkwiti lakini si ajabu tukamaliza miaka 10 watu hawaoni matunda ya mradi ule ambao Mheshimiwa Waziri mwenyewe amejionea kwa macho yake. Kwa hiyo nimwombe sana ule mradi utawasaidia wale watu ambao wanatembea kilomita 58 kutoka Mkwiti kwenda Tandahimba ni kilomita 58. Kwa hiyo nimwombe sana kwa unyenyekevu mkubwa, najua wanachapa kazi vizuri, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri lakini na watumishi wa Wizara ya Maji pia wanafanya kazi kwa usiku na mchana waone namna wanavyoweza kutusaidia. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)