Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nashukuru Mwenyezi Mungu kunijalia afya njema niweze kuzungumza machache yanayohusu maji hasa katika jimbo langu la Mtwara mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni nchi ya tano kwa kuwa na maji mengi ardhini leo hii, ni jambo la ajabu sana mpaka leo tunazungumza suala la maji, maji, maji, Tanzania kwamba tuna maji wakati ukichimba hata chini ya Bunge ndani yake huko kuna maji mengi kabisa maji baridi kabisa.

Mhrdhimies Mwenyekiti, kwa miaka mitatu hivi sasa kuna miradi mingi tumekuwa tunaizungumza miradi ya maji ya maji kwa mfano; mradi wa kwanza ambao ni mradi mkubwa sana tulielezwa ndani ya Bunge mwaka 2016 kwamba Serikali inataka kujenga Mradi mkubwa wa maji ambao utatatua kero ya maji katika majimbo ya Mtwara mjini, Jimbo la Mtwara vijijini na Jimbo la Nanyamba na huu mradi ni mradi wa kutoa maji mto Ruvuma kule Kitaya wenye gharama shilingi bilioni 200, mpaka leo huu mradi aujahanza na tulielezwa wakati ule kwamba huu mradi ni fedha za kutoka Benki ya Watu wa India Exim Benki ni mkopo lakini mpaka leo hatuelewe huu mradi umefikia wapi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kila mwaka unawekwa kwenye bajeti, kila mwaka unaelezwa kwenye vitabu vya bajeti kwamba kuna mradi mkubwa wa kuboresha majiji ikiwemo mji wa Mtwara, Mtwara Mjini lakini pia wilaya zile zingine ambazo nimeweza kuzitaja. Sasa tulikuwa tunaomba sana kwamba wakati huu mwaka huu ni mwaka wa nne sasa tunaenda tunahitaji miradi hii mikubwa iweze kutekeleza fedha zake ziweze kuletwa kwa ajili ya kuweza wananchi wetu kuondokana na tatizo la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine tulikuwa na mradi wa maji pale Mtwara mwaka jana zilipelekwa bilioni tano kasoro hivi huu mradi, ni mradi wa kutoa maji kutoka kule Kata ya Jangwani eneo la Lwelu na lengo lake ni kusambaza maji maeneo yale ambako mtandao wa Bomba haujafika. Sasa huu mradi nataka kumueleza Mheshimiwa Waziri hapa kwa sababu, Waziri hakuwepo wakati huu mradi tunaanza lakini Naibu Waziri alikuwe kwamba huu mradi wale wahusika wa maeneo yale ambapo visima vimechimbwa na tunashukuru kwamba tulifanya pump test maeneo yale maji yakapatikana mengi sana pale Lwelu, lakini kuna maeneo ambapo lile bomba limeweza kupitishwa lile bomba limepita mule wale wananchi wa maeneo yale mashamba yale hawajapewa hata senti tano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepigiwa simu sana wananchi wa maeneo yale wameniijia nyumbani zaidi ya mara kumi mara ngapi wakakaa wananiambia kwamba Mheshimiwa Mbunge tunataka utufikishie kilio chetu kwamba tunahitaji maji kweli wananchi wa Jimbo la Mtwara Mjini, lakini huu mradi wa bilioni tano inakuwaje kwamba Serikali imeleta huu mradi wamechukuwa mashamba ya watu wamechimba visima wamepitisha bomba lakini hawajapewa hata senti tano wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakaniambia Mheshimiwa Mbunge utufikishie kwa Mheshimiwa Waziri na nikaongea na Mheshimiwa Prof. Mbalawa nikamueleza Mheshimiwa Waziri tunakufahamu kwa utendaji wako mzuri ukiwa kwenye Wizara ile ya Mawasiliano ulikuwa unafanya kazi nzuri sana nilikueleza suala hili kwamba wananchi wa Jimbo la Mtwara Mjini ambapo huu mradi umepita hawajapewa hata senti tano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kujuwa naomba kuuliza hivi ni kweli kwamba wananchi wakipelekewa mradi eti kwa sababu wanashida ya maji hawa watu hawapewi fidia japo mashamba yao yamechukuliwa maeneo yale yamechukuliwa siyo kweli Mheshimiwa Waziri tunaomba Mheshimiwa Waziri ule mradi wa Lwelu ambapo unaenda kupeleka maji kwenye maeneo ya Kiolo maeneo ya Mbalawa chini kule, Magomeni, Chipuputa, Mitembo na maeneo yote ya Jimbo la Mtwara mjini hawa wananchi lile pomba lilipita wananchi walipwe fidia yao kwa sababu ni haki kulipwa fidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nilikuwa ninaomba kuzungumza siku nyingi tuna pitia taarifa kwamba Serikali imedhamiria kuondoa tatizo la maji katika jiji la Dar es Salaam na nizungumze tu kwamba sisi Wabunge wote ni wadau wa mji wa Dar es Salaam na sisi Wabunge la Kusini hasa hasa ni wadau wa maeneo ya Mbagala, maeneo yale ya Chamazi kule ndiko tunakoishi tukifika Dar es Salaam. Sasa haya maeneo yanatatizo la maji sana na kila mwaka inawekwa kwenye mpango kwamba tuna visima vya borehole ambayo vinachimbwa kule kibiji na maeneo mengi lakini inazungumzwa tu kila mwaka kuna visima visima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mtandao wa maji haujengwi kupelekwa maeneo ya Rangi Tatu, kupeleka maeneo ya Chamazi, kupeleka maeneo ya Mbagala kiujumla wake tunahitaji watu wale wa Dar es Salaam wapate kweli maji kwa sababu pale Kimbiji kuna maji mengi sana sana huu ni mwaka wa tatu tunapitia taarifa kwamba visima vimeandaliwa, visima vitapeleka maji lakini utekelezaji haupo Mheshimiwa Waziri tunaomba kwamba maeneo haya yapelekewe maji safari hii, hii miradi isiwe kizungumkutu kwamba inazungumzwa inatajwa inatajwa kila mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nilikuwa naomba kuzungumza hapa ni mradi wa Makonde, huu mradi ulijengwa na wakoloni mwaka 1953 na wananchi wa Wilaya ya Tandahimba, Jimbo la Nanyamba, Newala Kiujumla wake, wanashida ya maji sana, sana, pale Mtwara na huu mradi ndiyo suluhisho lakini kila mwaka inazungumzwa fedha zinazopelekwa ni fedha chache kila mwaka inaelezwa hapa kwamba tumetenga fedha kwa ajili ya kurekebisha mtandao maji yapo pale Makonde yapo mengi sana, lakini tatizo ni serikali kupeleka fedha ili yale Mabomba ili yaweze kurekebishwa na mashine iweze kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na tunaambiwa mashine iliamishwa kwenye mradi huu miaka hiyo ya nyuma iliamishwa mashine na kupeleka maeneo mengine sasa naomba kujuwa sisi wananchi wa kule wananchi wa Mtwara hatupaswi kutumia mashine ile ili tuweze kupata maji kwa hiyo, tunaomba Serikali kwa sababu Serikali ndiyo yenyewe ilifanya blunder ya kuondoa mashine ya mradi wa Makonde watenge fedha za kutosha ili wananchi wa Tandahimba, Newala, Nanyamba na Mtwara Vijijini wapate maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni mfumo wa maji taka kwamba kumekuwa na baadhi tu ya miji hapa Tanzania ndipo huu mfumo umeweza kurekebishwa au umeweza kutengenezwa. Lakini maeneo mengi ya mijini Tanzania huu mfumo wa maji taka ni mfumo muhimu sana kwa sababu, mfumo wenyewe wa watu wanavyoenda kuchimba vyoo vyao vile halafu hali inakuwa ni mbaya vikijaa inakuwa hali mbaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wananchi hawana fedha ya kukodi maboza kila siku kwenda kuondoa maji taka tunaomba sasa Serikali kuanzia Mji wa Mtwara Mjini hakuna kabisa huo mkakati yaani Serikali haituelezi. Nimekuwa nauliza kila mwaka hapa kwamba kwanini Serikali haiweki mfumo wa maji taka katika Mji wa Mtwara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sisi pale Mtwara Mjini tuko karibu na bahari sana gharama yake inakuwa ni ndogo na tunavyojuwa mfumo wa maji taka kwenye maeneo yenye vyazo maji vikubwa kama Bahari ya Hindi mifumo inaelekea huko baharini, kwahiyo tunaomba Serikali safari hii itenge kiasi cha fedha Mheshimiwa Waziri unanisikia Mheshimiwa Naibu Waziri unapiga kazi sana tunakusikia tunaomba mfumo wa maji taka Jimbo la Mtwara Mjini kwa sababu sisi tumekuwa tukipata shida sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nilikuwa naomba kuzungumza ni hili suala la wakala, wa wachimbaji wa visima wa ujenzi wa mabwawa. Mheshimiwa Waziri amezungumza vizuri sana hapa kwamba kuna huyu wakala, lakini jambo la ajabu huyu wakala ukitaka kuchimba kisima chochote kile hata ukiwa wewe ni Mbunge ukaenda ukawaeleza kwamba tunahitaji kuchimba kisima gharama wanazokupa ni kubwa sana na wananchi wa kawaida wanakuwa hawawezi kuwa-ford, kchukua hizi gari ambazo ni wakala wa Serikali gharama zake zimekuwa ni kumbwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wakati fulani nilikuwa natafuta maji Mtwara Mjini nikaenda kuwaeleza hawa mawakala lakini gharama walizonipa ilikuwa ni kubwa sana hata kama ni Mbunge niliweza, yaani sikuweza kuwa-ford zile gharama kwa hiyo watu wa kawaida, inakuwa ni hatari zaidi. Kwa hiyo, naomba kwa sababu lengo la Serikali ni kuwasaidia wananchi wa Tanzania, wananchi wa vijijini waweze kupata maji maeneo ambako hakuna vyanzo vya maji, lakini hizi gari za wakala zinaweza zikachimba visima virefu na visima vifupi gharama ziwe nafuu ili wananchi waweze kuwa-ford. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)