Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia hoja hii ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya. Pili, naunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende moja kwa moja kwenye mchango wangu nikianza na fedha za maendeleo kwenda kidogo. Nikiangalia mwaka 2015/2016, fedha za maendeleo zilizokwenda ni asilimia 28; mwaka 2016/2017 zilikwenda asilimia 25 na mwaka 2017/2018 zilikwenda asilimia 22. Ukiangalia huo mtiririko unaona kabisa Wizara hii inazidi kwenda chini na kwamba wananchi watazidi kupata matatizo siku hadi siku badala ya kwenda juu inakwenda chini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo haitoshi, kwenye ripoti ya CAG inaonesha kwamba fedha zilizokwenda kwenye Bodi ya Mabonde ya Maji ambapo zilipangiwa kwenda shilingi bilioni 49.5 kwa mwaka 2016/2017 lakini zilikwenda shilingi bilioni 6.6 tu, sawa na asilimia 13 tu. Fedha ambazo hazikwenda ni shilingi bilioni 42.9, sawa na asilimia 87. Tukiangalia mwaka uliofuata wa 2017/2018 kati ya shilingi bilioni 38.4 zilizoidhinishwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo zilikwenda shilingi bilioni 7.2 tu, sawa na asilimia 19 ya bajeti yote ya mwaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza, je, Serikali ina dhamira kweli ya kumtua mama ndoo kichwani? Kwa sababu tumekuwa tukiimba kwamba Serikali inataka kumtua mama anayetaabika ndoo lakini kwa mtiririko huu tutafika kweli? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia upotevu wa maji, ni mkubwa sana ambao umesababisha hasara ya shilingi bilioni 47.18. Ukiangalia mikoa 15 yenye upotevu wa maji ambayo imeoneshwa kwenye ripoti ya CAG, tukianza na Mkoa wa Njombe ambao inaonesha hapa kiasi cha upotevu wa maji kisichokubalika shilingi milioni 196.2. Tukija Mwanza ni shilingi milioni 677.52 na mikoa mingine imeorodheshwa hapa ambayo jumla yake inakuja shilingi bilioni 47.18. Wakati huo huo tunaongelea juu ya uhaba wa maji. Upande mwingine tunaona upotevu wa maji upande mwingine tunaona uhaba wa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali iweke mfumo ambao utasaidia kupunguza upotevu huu wa maji. Niishauri Serikali wale wanaokwenda kusoma mita za maji basi wawe na wajibu wa kuhakikisha wanaangalia mabomba au miundombinu ambayo inatoa maji ambayo inavujisha maji kwa sababu kuna upotevu mkubwa sana wa maji, nikianza hapa hapa Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakaa kisasa nimeshawasilisha hii hata mwaka jana kwamba kuna mabomba yana tiririsha maji na nimeenda kuripoti mara nyingi huko kwenye mamlaka ya maji DUWASA juu ya upotevu wa maji huu, lakini ukija siku inayofuata unaona maji bado yanaendelea kutiririsha, sasa kama hapa Dodoma ipo hivi hayo maeneo mengine inakuwaje? Kwa hiyo niiombe Serikali ifuatilie suala hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala lingine ni suala la wateja kutokuwa na mita za maji kuna wateja wengi ambao hawana mita za maji matokeo yake, unakuta bill zinakadiriwa juu na mtu anaendelea kutoa bili hizi maana hajuwi sasa nitoe mfano halisi mimi wazazi wangu walikuwa kila mwaka wanatozwa pesa nyingi sana mwaka huu nikashtuka nikasema haiwezekani hizi bili ni kubwa sana nikaenda kufuatilia, nikakuta hawana mita nikawauliza watu mamlaka ya maji kwanini hamjawawekea mita hawakuwa na chakuwaeleza, kwa hiyo niombe Wizara ifuatilie suala hili kuhakikisha wateja wote wanapata mita za maji, kusudi watu walipe hela kwa uhalali wasizidishiwe na wala isiwe chini zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la uhaba wa maji kwa ujumla.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Malizia kengele ya pili hiyo.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Niombe Wizara ifuatilie suala hili kwa sababu kuna maeneo ambayo tulikuwa tukiimba kila siku hapa kwamba tunaomba maji kwa mfano kuna kijiji cha Itengelu huko Wanging’ombe huko nyuma walikuwa wanamaji mengi tu kwenye bomba mpaka mabomba toka mabomba yamekufa sasa hivi wanahangaika hawa wananchi wanachota maji machafu kwa kilometa nyingi naomba Wizara ifuatilie suala hili. Ahsante sana.