Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. WILLIAM V. LUKUVI: Kwa kuwa Jimbo la Isimani lina shule zaidi ya 50 za msingi na 13 za Sekondari na lipo vijijini, vijana wengi wanaomaliza sekondari hawana chuo chochote cha mafunzo ya ufundi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Isimani ndilo lenye eneo lote la Ruaha National Park na wazalishaji wakubwa wa mazao ya kilimo hususan mpunga. Pia wana nia ya ujenzi wa nyumba bora, hivyo kuwapo kwa Chuo cha Ufundi chini ya VETA itasaidia vijana wa Iringa vijijini hususan Jimbo la Isimani kujifunza masomo ya ufundi mbalimbali na masomo ya utalii na hoteli. Kwa hiyo, naomba sana Wizara ikubali kujenga Chuo cha Ufundi – VETA Jimboni Isimani wilaya ya Iringa Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.