Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kuipongeza Wizara kwa wasilisho zuri na jithada zinazofanywa kuboresha elimu. Pamoja na pongezi hizi, nina mchango kidogo kwa baadhi ya maeneo. Elimu yetu ilenge kuibua na kukuza vipaji hasa mashuleni. Kuna watoto tangu shule ya msingi wanaonyesha vipaji vikubwa sana. Laiti watoto hawa wangetiliwa maanani wakaendelezwa kwa namna ya tofauti wangekuja kusaidia sana Taifa letu. Utakuta mtoto ana akili sana ana kipaji fulani lakini wazazi kwa kukosa uwezo mtoto yule anaishia njiani. Hivyo, tunajikuta tunapoteza rasilimali kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni mazingira mazuri ya kusomea. Kuna tatizo ambalo kwa sasa tunaweza tusilione ila baadaye likawa janga la Taifa. Watoto wamekuwa wakibeba mabegi yenye mzigo mzito sana kutokana na kutokuwa na ratiba maalum. Serikali ingeangalia uwezekano wa kujenga angalau makabati au kuhakikisha kunakuwa na ratiba maaum na zinafuatiliwa ili kuepusha matatizo ya uti wa mgongo yanayoweza kuwapata watoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, waalimu wawe motivated hasa katika mishahara, mathalan wanapofanya kazi kijijini, mshahara uwe juu zaidi ya aliye mjini ili kuondoa tatizo la walimu wengi kukwepa kwenda vijijini. Shule za boarding watoto wanahitaji sana uangalizi. Watoto wengi wanaanzisha mahusiano yasiyofaa. Hili lifanyiwe utafiti na awepo mtu wa kuwaangalia watoto hawa hasa kipindi cha usiku. La sivyo, watoto wataendelea kuharibika mashuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia suala la taulo za kike hasa vijijini ni muhimu kwani watoto hawapati nafasi ya kusoma vizuri. Mfano shule unakuta haina vyoo vya kutosha, haina maji kiasi kwamba mtoto katikati ya masomo anaweza kwenda kujisitiri kwa wale wanaotumia njia nyingine zaidi ya pad, hivyo kuamua kukaa nyumbani mpaka pale atakapomaliza siku zake. Hivyo, kukosa masomo kwa kipindi chote hicho na wengine wanaenda hadi siku saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijana wengi kwa kukosa uwezo wa kifedha kwa wazazi au walezi wao wamejikuta hawana uwezo wa kufika kidato cha nne na kuendelea kwa kujibana na kuhangaika sana. Unakuta wanapata nafasi ya kujifunza ufundi stadi, udereva na ni katika vyuo vyetu vinavyotambulika kama VETA, NIT lakini linapokuja suala la ajira rasmi wanakosa sifa. Serikali iwaangalie sana hawa vijana na wengi wao wana vipaji vikubwa na ufanisi mkubwa. Iangaliwe ni jinsi gani wanaweza kuajiriwa au kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bure bado ina changamoto nyingi sana. Kuna wazazi, walezi wengine hawana hata uwezo wa kununua sare za shule, madaftari, vitabu na nauli ili watoto hawa waweze kufikia hiyo elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.