Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ina upungufu mkubwa sana wa Walimu na uhaba wa Walimu hasa Walimu wa Sayansi. Vilevile Walimu wa kike, tunaomba Serikali ituongezee Walimu kwani kutokana na tatizo hili mara nyingi Halmashauri hii inakuwa chini sana katika ufaulu wa wanafunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo shule shikizi zifuatazo ambazo zimeanzishwa na kujengwa kwa nguvu za wananchi, lakini Serikali inachelewa kuzifungua na kusababisha watoto wengi kutosoma. Shule hizo ni Kirando na Karanda. Tunaomba shule hizo zifunguliwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashauri Serikali kupandisha madaraja ya walimu ambapo ni kwa muda mrefu hawajapandishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kulipa posho ya mazingira magumu kwa Walimu. Serikali itoe posho kwa Walimu wanaofundisha katika mazingira magumu ya Vijijini kusiko na barabara nzuri, kwani wanatembea umbali mrefu kufuata huduma. Pia wapandishiwe mishahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya shule za Sekondari za Kata bado hazijapelekewa vifaa licha ya kuwa na majengo ya maabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo la kukosekana kwa mabweni hasa kwa watoto wa kike ambao wanatembea umbali mrefu unaowasababishia kukumbana na vishawishi vingi na hatimaye kushindwa kuhitimu masomo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga mkono hoja.