Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA), ni muhimu kukawa na mtawanyiko mzuri zaidi nchi nzima ili kuwapatia wahitimu husika Form IV, STD VII, hata Form VI wasiopata fursa nyinginezo “Alternative Route” kuelekea maendeleo binafsi na Taifa kwa ujumla. Wilaya ya Tunduma iko mpakani, ni ya siku nyingi (1905) na iko mbali na Vyuo vya aina hiyo, (ukiacha chuo kimoja tu binafsi ambacho access ya wananchi wengi ni limited kutokana na gharma kuwa juu. Tunaomba Wilaya hii ipewe kupaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Serikali inaendelea kukamilisha taratibu za kuwaajiri Walimu waliohitimu katika vyuo na ngazi mbalimbali na wakati kuna uhaba mkubwa wa walimu katika shule zetu, napendekeza Serikali iweke utaratibu wa kuwapa mikataba ya muda mfupi mfupi walimu hao kwa “kujitolea.” Ni wazi kutajitokeza mahitaji ya Resources kidogo. Hata hivyo, wapo baadhi watajitokeza kufanya hivyo. Wanachohitaji ni kutambuliwa na kuwafanya wawe active katika taaluma. Inawezekana pia “motisha” ikawa ni kupata kipaumbele ajira zinapojitokeza.