Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kutupatia fursa ya Elimu Bure. Pamoja na kusaidiwa na Serikali, tuna shule ambazo ni za zamani sana hasa Mbulu DC mfano Shule ya Msingi Maskaroda inahitaji ukarabati kwani majengo yake ni ya zamani, tangu 1955 na watoto ni wengi. Tunaomba Wizara ione namna ya kusaidia ujenzi wa madarasa. Pia katika Sekondari wananchi wa Maretadu wamejenga Sekondari ya Kidato cha Tano bwalo na madarasa manne. Tunaomba msaada wa kuongeza bwalo kwani wananchi wameamua kuchangia majengo ili kusaidia kuanzishwa kwa Kidato cha Tano na Sita Mbulu DC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule maalum zipewe kipaumbele katika bajeti ya Waziri wa Elimu kwani bila kufanya hivyo wanasahaulika sana. Hivyo naomba zipewe kipaumbele. Mfano, Shule ya Viziwi Dongobesh na nyingine zilizomo katika nchi. Walimu wanahitajika sana katika shule hizi za walemavu hasa wale wenye ujuzi wa kuunda hao watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo Sekondari Mbulu DC zimejengwa na wananchi, zinahitaji msaada wa kujengewa madarasa na nyumba za walimu, mfano Dr. Olsen Sekondari ina wanafunzi wengi na hawana madarasa na bweni; na watoto wa Kidato cha Tano na Sita wanapata taabu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto za Walimu wa Sayansi ni kubwa sana katika Shule nyingi za Sekondari, hivyo kupelekea ufaulu kuwa chini. Hivyo tunaomba Walimu wa Sayansi waongezwe ili kukidhi haja hiyo.