Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, naunga mkono mia kwa mia utendaji wa Waziri na wasaidizi wake wote. Nachoomba kwenye jimbo langu ni kuimarisha chuo kipya cha VETA Paramawe kwa vifaa ili kiweze kusaidia vijana wa Nkasi na Mkoa wote wa Rukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ni muhimu Wizara ione uwezekano wa kuongeza majengo kwa kuwa tuna kiwanja cha ekari zaidi ya hamsini. Pia ikiwezekana chuo kiwezeshwe kutoa kozi zote zinazotolewa na vyuo vingine vya VETA nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kukupongeza Prof. Ndalichako na wasaidizi wake wote, tuko pamoja.