Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali na Wizara kwa jitihada kubwa za kuinua elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukitaka kuinua elimu basi ni lazima Serikali iwe na mkakati wa kuongeza idadi ya walimu hasa maeneo ya vijijini, hii inaendana na kuboresha miundombinu ya maeneo ya vijijini. Walimu wengi wanaondoka maeneo ya vijijini kwa sababu tu ya miundombinu mibovu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walimu wengi wanadai haki zao, hili pia ni tatizo. Serikali lazima ijitahidi kuhakikisha stahiki za walimu zinalipwa kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, pale Handeni kuna Chuo cha FDC. Chuo hiki kina msaada mkubwa sana kwa Mkoa wa Tanga. Naiomba Serikali ikiangalie kwa jicho la karibu kwa kuwa hali yake ni mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.