Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami napenda nichangie Wizara hii muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa uboreshaji wa miundombinu ya elimu katika shule za msingi na sekondari hususani mabweni, madarasa na majengo ya utawala katika Shule ya Msingi Gongali na Sekondari za Endabash, Banjuka, Welwel na Mangola.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya wanafunzi wa elimu ya juu hawapati mikopo na hivyo kuhangaika sana. Niishauri Serikali kuboresha mifumo ya utoaji mikopo ili kweli wale wanaostahili wapate mikopo hiyo. Wako wanafunzi wameacha masomo baada ya kukosa ada, vipo pia vyuo vikuu vinawakaririsha wanafunzi mwaka endapo atashindwa kukamilisha ada, hii si sawa kabisa. Wanafunzi wote wa elimu ya juu wapewe nafasi ya kukopa kisha utaratibu wa kulipa uimarishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya ufundi na mafunzo ya VETA hayaepukiki katika Tanzania ya Viwanda tunayojenga. Serikali imesema itajenga Chuo cha Ufundi katika kila Wilaya. Halmashauri ya Wilaya ya Karatu imejenga Chuo cha Ufundi cha kisasa. Tunashukuru Chuo kimesajiliwa lakini bado kinakosa wakufunzi na vifaa. Tunaomba Wizara itusaidie kupata wakufunzi na vifaa vya ufundishaji katika Chuo cha Ufundi cha Christimac Tree, Bashay Karatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri pia Serikali irudishe mfumo wa zamani wa shule zote za msingi na sekondari kuwa chini ya Wizara ya Elimu badala ya kuwa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Kwa muundo wa sasa, shule hizi ni kama hazina mwenyewe, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ina mambo mengi sana na hivyo kupelekea eneo hili la elimu kutozingatiwa ipasavyo.