Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, mwandiko wa kuunganisha herufi. Katika hili, Serikali inabidi iangalie upya mpango huu kwani umekuwa ukileta mkanganyiko kwa wanafunzi wa madarasa ya chini yaani awali mpaka darasa la nne kwa namna ambavyo imekuwa ikiwaletea taabu wanafunzi katika utambuzi wa herufi na namna ya kuanza kuzitambua na hivyo kuwa na mwandiko mbaya. Hivyo basi, Serikali kupitia Wizara hii iangalie namna nzuri ya uumbaji wa herufi toka wanafunzi wakiwa katika hatua za awali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, maabara za shule za sekondari. Ni vema sasa Serikali ikaelekeza nguvu ili kumalizia maabara za shule zote nchini na kuhakikisha zinanza kufanya kazi kwani tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda. Hivyo, ni vema maabara ziboreshwe na kumalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, maktaba. Serikali sasa ni lazima itambue umuhimu wa maktaba kwani ndiyo chanzo cha kufanya rejea ya mambo mbalimbali ambayo wanafunzi wanakuwa wanafundishwa darasani kwa muda mfupi. Hivyo basi, Serikali iharakishe ujenzi wa maktaba katika shule zote za msingi na sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, nilileta ombi la Shule ya Sekondari Mpanda ianzie Form I – VI badala ya ilivyo sasa form four - six. Je, ombi hilo limefikia wapi na limeshughulikiwa kwa kiasi gani?