Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niongelee kuhusu mikopo ya vyuo. Vyuo vingi viliahidi utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi hasa udaktari kwa kupata mikopo asilimia 100 lakini wanafunzi wengi hasa wasichana wameacha kozi au kubadilisha kwa ukosefu wa ada.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, majengo ya shule za zamani. Majengo mengi yamechakaa japo kuna mengine yamefanyiwa ukarabati. Naomba speed iongezeke ili kuweka mazingira mazuri ya watoto wetu kusoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, viongozi wa vyuo. Kumekuwa na uteuzi wa maprofesa wengi kumsaidia Rais kazi za siasa na kuacha ombwe kubwa katika sekta ya elimu. Tunaomba kama hakuna haja wangeachwa waendelee na kazi ya kufundisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, siasa vyuoni. Kumekuwa na upendeleo kwa vijana wetu vyuoni kwa kuangalia vyama. Vyuo kama DUCE na Mwalimu Nyerere wanatoa kumbi zao kwa vijana wa CCM ili kufanya siasa wazi na kuleta mgawanyiko kwa vijana wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, pads. Tunaomba punguzo la bei za taulo za kike na zitolewe kwa wanafunzi husika kwa kutenga fungu na kusaidia tozo ili zifike kwa walengwa.