Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Elimu kwanza naomba kukujulisha kuwa binafsi ni mhitimu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere zamani kivukoni. Mheshimiwa Waziri hebu tusaidie kutatua hoja hii, hivi karibuni Mheshimiwa Waziri Mkuu alitembelea Chuo cha MNMA akiwa ameongozana na wewe Waziri na kukuagiza kuwa wizara ifanye mchakato wa kukipandisha hadhi chuo hiki na kuwa chuo kikuu. Je, mmefikia wapi hadi leo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku mbili tu baada ya agizo lile la Waziri Mkuu, nikauliza swali la msingi hapa Bungeni kuhusu hoja hiyo hiyo ya kupandisha hadhi chuo hiki lakini majibu ya wizara yako yalionyesha kutokubaliana na hoja ya kukipandisha hadhi chuo hiki na kuwa chuo kikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nadhani ni muda muafaka sasa chuo hiki kipewe hadhi ya kuwa chuo kikuu ili kuendeleza fikra pevu za hayati Mwalimu Nyerere. Nchi za wenzetu waasisi wa mataifa yao wamewaenzi kwa kuvipa majina ya vyuo vyao mfano mzuri ni Nelson Mandela University, Kwame Nkurumah University , Kenyatta Universtity, MOI University etc. naomba chuo hiki kwa umuhimu wake kipandishwe hadhi kuwa chuo kikuu.

Jambo la pili ni shule ya Sekonari Mchinga kupandihswa hadhi na kuwa shule ya kidato cha tano na sita. Wilaya yetu ina shule moja tu ya kidato cha V na VI nayo ni Maliwa Sekondari iliyopo Jimbo la Mtama. Lakini Jimbo la mchinga halina shule ya kidato cha V na VI hata moja. Tafadhali ninaomba wizara itusaidie kwa kutenga fedha za nyumba za walimu na sisi tutajenga mabweni ili shule hii ipandishwe na kuwa ya kidato cha tano na sita. Ahsante.