Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa hii. Nianze kwa kuunga mkono hoja hii sambamba na kumpongeza mtoa hoja kwa wasilisho zuri lenye kuleta matumaini kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Wilaya ya Mafia kwa kushirikiana na Mbunge wao, Mheshimiwa Mbaraka Kitwana Dau wamefanikiwa kujenga Chuo cha Ufundi (VETA) na ujenzi wa Chuo hicho umekamilika takribani miaka minne iliyopita. Chuo hiki hadi sasa hakijapata usajili kutoka mamlaka husika kwa zaidi ya miaka miwili na nusu sasa. Moja ya hoja iliyotolewa ilikuwa ni kukosekana kwa umeme katika Chuo hicho. Ninayo furaha kulifahamisha Bunge lako Tukufu kuwa suala la umeme limeshatatulika baada ya wakala wa umeme vijijini kufikisha umeme katika chuo hicho na unawaka hivi sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mafia ina shule sita za Kata. Kati ya shule hizo, zote zina tatizo la hostel za wanafunzi ukiondoa shule moja tu, shule ya sekondari ya Kitomondo. Tunatambua changamoto ya ufinyu wa bajeti. Tunaiomba Serikali itusaidie Mabweni ya wanafunzi kwa shule za Kirongwe, Baleni na Micheni. Shule hizi zina dahili wanafunzi kutoka maeneo ya mbali hususani maeneo ya pembezoni kwenye visiwa vidogo vidogo vya Juani, Chole na Jibondo. Inawawia tabu kupanda vyombo vya Mashua na Boti kwenda na kurudi majumbani ukizingatia nyakati za pepo kali za Kusini na Kaskazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na naunga mkono hoja.