Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe mchango wangu kwa maandishi katika wizara hii. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri pamoja na watendaji wake wote kwa kazi nzuri sana wanayoifanya na kuitendea haki wizara hii ambayo ni muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Prof. Joyce Ndalichako anastahili pongezi kubwa kwani mwenye macho haambiwi tazama na mwenye masikio haambiwi sikia. Changamoto nyingi zilizokuwepo zimepungua kwa kiwango kikubwa lakini pia elimu imeboreka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri na kubwa ambazo zimekuwa zikifanyika bado kuna changamoto ambazo zinaweza kuboreshwa mfano kurudisha michezo, kilimo na mchakamchaka mashuleni haya huko miaka ya nyuma yalikuwepo na matokeo mazuri yalionekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara sasa iandae mfumo mzuri wa kuwaandaa wanafunzi kisaikolojia kwani wanafunzi wengi wanaomaliza akili yao ni kupata ajira ambazo kupatikana si rahisi sana kiasi kwamba akikaa miaka mingi nyumbani bila kupata ajira anakata tamaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba katika mchango nitoe salamu kutoka kwa wananchi wa Kalenga walionituma nimfikishie salamu za kushukuru sana Waziri wa Elimu Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako kwa kuikumbuka shule ya msingi Kongwe ya Kalenga kwa kuwajengea maboma mawili ya madarasa yenye madarasa manne na uzio wa kuizunguka shule na matundu 16 ya vyoo pamoja na kukarabati nyumba za walimu ambazo zilikuwa zimechakaa kabisa na kushindwa kukaliwa na walimu hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali yangu sikivu kuwapatia Wizara ya Elimu pesa yote iliyoombwa katika bajeti yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.