Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, uhaba mkubwa wa miundombinu katika shule za msingi na sekondari nchini, bado kuna changamoto katika Sekta ya Elimu hususani katika miundombinu na hii inapelekea kushuka kwa ufaulu na kusababisha walimu kuishi katika mazingira magumu na huku ni jukumu la Serikali kuhakikisha inatatua kero zao, hakuna Elimu bila walimu hivyo Serikali hii itatue kero ya nyumba bora kwa walimu wa Shule ya Msingi na Sekondari mapema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabweni, Shule ya Sekondari Mpanda Girls mpaka sasa haina uzio na shule inayotegemewa na wananchi kwa ufaulu wake, shule hii iko nje ya mji kidogo na imezungukwa na shughuli za kiuchumi stendi ya malori na mabasi makubwa soko na kilimo je? Hii shule ni ya wasichana kuzungukwa na shughuli hizi na pia shule haina uzio hamuoni kuwa Serikali inahatarisha usalama wa watoto na mimba kwa wanafunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viboko, shule hii, imezungukwa na bwawa na mito wakati wa usiku viboko wamekua wakizunguka kwenye maeneo ya mabweni na kuleta hofu kwa wanafunzi. Naiomba Serikali ione namna ya kutatua jambo hili kabla halijaleta madhara.