Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, je ipi sera ya elimu yetu ya sasa na inalenga kuandaa wahitimu wenye weledi gani?

(i) Ngazi ya elimu ya msingi?

(ii) Ngazi ya kidato cha IV?

(iii) Ngazi ya kidato cha VI?

(iv) Ngazi ya chuo kikuu?

Sera ya nchi yetu inakidhi kweli mahitaji ya soko? Mbona kama kuna ombwe la maandalizi? Rejea idadi kubwa ya wahitimu wasio na ajira katika ngazi zote walizohitimu. Kwa nini tusibadilishe mtizamo wa elimu yetu? Nashauri kuitishwe mjadala wa kitaifa, tupate maoni mbalimbali juu ya mfumo wa elimu uliopo na kama kweli bado unakidhi haja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini tathmini ya Serikali na mfumo wake wa elimu ya 7.4.2? Ukilinganisha na Kenya ya 6.2? Serikali haioni umuhimu wa kupunguza muda mrefu wa vijana kukaa elimu ya msingi wakati haiwapi ujuzi specific?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ione kuwa huu ni wakati muafaka wa kufufua elimu za kujitegemea shuleni kwa nguvu na kasi ile ile kuondoa changamoto ya kuzalisha watoto wasio ajirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Elimu juu ya mfumo wa mitihani ya mwisho kama kipimo cha ufaulu/daraja la kuvuka hatua nyingine iangaliwe upya. Mfumo utengenezwe vizuri ili kuwe na mfumo wa kutathmini ufaulu kwa kuwa kipimo cha mtihani wa mwisho hakiakisi uelewa wa mtoto/ mwanafunzi; hii ni kwa sababu siku za mtihani zinakuwa fixed/ tension ya mtihani na mambo mengine yanaweza kupelekea mtoto ku-fail wakati amekuwa akifanya vizuri katika kipindi cha kujifunza. Nashauri badala ya final exams tujikite kwenye collective assessment and final exams iwe sehemu yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwepo kwa masomo mengi kwa wanafunzi katika ngazi zote, kuanzia darasa la kwanza hadi la saba. Hii inaweza kuanza kama proposal na ingependeza ikapendeza kufanyika kwenye block yote ya EA.