Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ZAINABU M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako Mbunge, pia Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa pamoja na wasaidizi wake kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuyatekeleza majukumu yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri, wanafunzi wanaoenda kusomea fani ya ualimu wawe na vigezo vinavyohitajika kitaaluma, kwa sababu baada ya mafunzo ya ualimu wataenda kutoa elimu kwa watoto na jamii. Hivyo isiwe mazoea kwa mwanafunzi aliyepata division III au IV ndio aende kusomea kozi ya ualimu. Hivyo nashauri Serikali izingatie hili wachukue wanafunzi waliofaulu kuanzia division one na two. Ili kuleta tija katika elimu.

Naishauri Serikali ili kuweka msingi mzuri katika elimu mitaala iwe na masomo ya ziada kama ilivyokuwa katika miaka ya 1980, mfano Morogoro sekondari mitaala yetu ilikuwa unasoma masomo ya ziada (woodwork, cookery, needle work, metal work, fineart) pamoja na masomo yote ya kawaida. Hivyo mwanafunzi ndani ya miaka minne anakuwa na msingi wa kupata mafunzo ya masomo ambayo baada ya hapo kama hakupata nafasi ya kuendelea na kidato cha V – VI, atakuwa na uwezo wa kujiajiri kutokana na masomo ya ziada aliyosomea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali irudishe mitaala ile katika shule zetu za sekondari kuanzia kidato cha I – IV. Naishauri Serikali fedha zifikishwe kwa wakati ili kuweza kutekeleza majukumu kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna uhaba wa zana za kufundishia teaching aids, katika shule zetu. Nashauri Serikali itenge fungu la kutosha ili shule zetu ziwe na zana za kufundishia ili mwanafunzi aweze kuwa na uelewa zaidi katika somo analofundishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna uhaba wa nyumba za walimu hususani maeneo ya vijijini. Hivyo nashauri Serikali ijenge nyumba za walimu maana hutembea umbali mrefu sana kutoka walikopanga nyumba zao hadi kufika katika shule afundishayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokuwa na wakaguzi mara kwa mara katika shule zetu, nashauri Serikali iwe na vitendea kazi vya kutosha mfano magari ili kuwawezesha wakaguzi kufika kwa urahisi katika maeneo husika ya shule na sio kutoa taarifa ambazo si za uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhaba wa walimu hususani katika shule zilizopo vijijini. Naishauri Serikali iweke miundombinu mizuri na motisha nzuri kwa walimu wanaofundisha shule za vijijini ili kuweza kuwavutia walimu wengi kufundisha vijijini na sio kukimbilia mijini kufundisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iweze kutoa semina mbalimbali kwa walimu ili kuweza kuwajengea uwezo katika sekta hii na kujua wajibu na majukumu yao ya kila siku. Pia waweze kuwalea wanafunzi kwa maadili mema ya kiutamaduni wa mtanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhaba wa vyumba vya madarasa, hii hupelekea mlundikano wa wanafunzi katika chumba kimoja cha darasa, na humuwia vigumu mwalimu kuwafikia kuwafundisha wanafunzi wengi kwa wakati mmoja. Nashauri Serikali ijenge vyumba vingi vya madarasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iongeze mishahara kwa walimu na wakufunzi ili waweze kutoa elimu kwa usahihi. Maana wengi wanakuwa na msongo wa mawazo na kushindwa kufundisha vizuri wanafunzi wetu na matokeo yake wanafunzi hufeli katika masomo yao. Wakiongezewa mishahara na posho mbalimbali watahamasika kufundisha kwa weledi mkubwa zaidi na kupelekea wanafuzni kufaulu na kuwa na Taifa lenye watu waliopata elimu bora.