Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kumshukuru Mungu kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja hii ya elimu kwa maandishi. Hospitali ya MUHAS Mloganzila ilianzishwa kwa madhumuni ya rufaa na pia, teaching hospital ilikuwa kujengwe hostel na nyumba za Madaktari na wataalam wengine, ili kuwezesha huduma kupatikana kwa urahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali hii ya Mloganzila imeanza kutoa huduma, lakini Madaktari wanaotakiwa kutoa huduma wanasafiri kutoka makazi yao, wengine maeneo kama Mbagala kwa muda mrefu njiani mpaka Mloganzila. Watumishi hawa hawapewi msaada wowote kama petroli/ nauli kuwawezesha wafike kwenye kituo cha kazi. Matokeo yake ni kuwepo kwa upungufu mkubwa wa Madaktari na wataalam wengine wa afya. Ni muda muafaka sasa changamoto hiyo ya makazi ikapatiwa ufumbuzi na kwa muda huu wapatiwe nauli/mafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Madaktari Bingwa waliofika miaka 65 wanapewa mikataba ya muda mfupi na wakati mwingine hata malipo yao yanasuasua na hawalipwi kwa wakati. Huu ni udhalilishaji wa wataalam wetu waliotumikia Taifa hili kwa muda mrefu. Wanafunzi wanaohitimu kwenye vyuo vikuu vya tiba, wengi wao hawana interest ya kufundisha, wengi wanakwenda kwenye public health na wengine nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha Madaktari Bingwa waliofikisha umri wa miaka 65 Wizara imeshindwa kuwatumia vizuri. Kwa nchi za wenzetu hawa ndio hazina kubwa ya Wahadhiri, wanafundisha mpaka uzeeni kabisa. Kwa sasa Madaktari Bingwa hawa wamehamia vyuo vya tiba binafsi/kanisa kama Bugando na KCMC, wengine wanakwenda nje ya nchi Botswana, Namibia, South Africa na kadhalika. Hivyo, muda si mrefu MUHAS itakuwa 3rd class teaching institution.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba, Wabunge wengi waliweka ukomo wa wataalam bingwa kuwa miaka 65, naishauri Serikali, ili kutumia hazina hii ya wataalam wapewe angalau mikataba ya miaka miwili-miwili na kulipwa gratuity kila wanapomaliza miaka yao miwili. Utakubaliana nami kwamba, umri wa kuishi umeongezeka, hivyo mtaalam bingwa wa miaka 65 bado ana nguvu kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.