Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza kazi nzuri sana inayofanywa na Bodi ya Mikopo hasa ufuatiliaji wa madeni, lakini pia na huduma nzuri hasa ofisi yenu ya Dodoma watumishi na meneja wao wanasikiliza hongera sana. Hata hivyo, wapo walipaji ambao wameshamaliza mikopo ambayo walikatwa zaidi ya walichokuwa wanadaiwa ambapo sasa ile fedha kurejeshwa inasumbua sana. Nashauri sana inapotokea hivyo wahusika warejeshewe zaidi yao ili waendelee kuwa Mabalozi wema wa Bodi ya Mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili kuna suala la majina kufanana pamoja na kuwa marejesho hufanywa kwa kutumia check number, zipo cases ambazo kutokana na majina kufanana kunatokea nyakati makato ya mtu A anakatwa mtu B na yale ya B anakatwa A and vice versa. Nashauri Bodi iliangalie hili ili kuondoa mtu kukatwa mara mbili na mwingine kutokatwa marejesho. Ahsante.