Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Wizara ya Elimu kwa kazi kubwa wanayoifanya. Elimu; iko haja ya kuangalia au kupitia upya mitaala yetu na Sera ya Elimu ili kuwaandaa wanafunzi kwa level mbalimbali kujiajiri na sio tu kutegemea kuajiriwa, elimu ya stadi za maisha iwekewe mkazo zaidi. Katika maeneo mengi mwananchi wamejitahidi kujenga mabomba kwa ajili ya madarasa na maabara, Serikali iangalie namna ya kuwasaidia wananchi hawa kumalizia majengo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukarabati wa shule kongwe. Serikali imefanya ukarabati wa shule kongwe za sekondari, zipo shule za msingi kongwe na zenye hali mbaya zinahitaji ukarabati mfano kwenye Jimbo la Korogwe vijijini ipo Shule ya Msingi ya Madela Ratuba, shule hii ilijengwa mwaka 1952 na haijafanyiwa ukarabati kwa muda mrefu. Niombee Wizara isaidie ukarabati wa shule hii pia ipo Shule ya Msingi Ng’anzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya ufundi; naiomba Serikai imaarishe elimu ya ufundi. Kwenye Jimbo la Korogwe Vijijini tuna Chuo cha Ufundi Mnyuzi, chuo hiki kikipanuliwa, kikapewa vitendea kazi na kuongeza aina ya course zinazotolewa kitasaidia sana wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo kwa mfumo wa elimu ya shule. Chuo hiki kinaweza kusaidia wanafunzi wengi sana wa Wilaya za Korogwe, Lushoto, Muheza na hata Handeni. Naomba sana Wizara itusaidie kuboresha, kupanua na kuimarisha chuo hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Mikopo; bado kuna manung’uniko ya baadhi ya Watanzania maskini kukosa mikopo kwa ajili ya kugharamia elimu ya juu. Ni vyema Bodi ya Mikopo ikaangalia hili lakini pia tayari kufanya marekebisho hata katikati ya masomo.