Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza viongozi wa Wizara hii ikiongozwa na Waziri Mheshimiwa Profesa Ndalichako, Naibu Waziri Mheshimiwa Ole-Nasha na Katibu Mkuu Dkt. Akwilapo. Nawapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya na mabadiliko chanya yanaonekana kwenye sekta hii ya elimu. Mchango wangu utajikita kwenye maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kitengo cha Udhibiti Ubora wa Elimu (Ukaguzi wa Shule), kitengo hiki kipewe rasilimali za kutosha ili kitekeleze majukumu yake, wapewe rasilimali fedha na watumishi. Kitengo hiki kibadilishwe muundo, badala ya kuwa na ofisi ya kanda sasa zifunguliwe kwenye mkoa. Ofisi za kanda ziliweza kudumu wakati idadi ya shule za sekondari ni chache, kwa sasa idadi imeongezeka na hawawezi kukagua shule zilizopo kwenye kanda husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Matumizi ya TRC (Teachers Resource Centre), huko nyuma tulikuwa na program ya DBSPE (District Based Support to Primary Education) na kulikuwa na mtando wa TRC ambazo zilitumika kutoa mafunzo kazini kwa Walimu wetu. Naomba vituo hivi vitumike kama lengo lake lilivyokuwa hapo awali. Vitengewe fedha za kutosha ili viweze kuendesha semina za Walimu katika maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taasisi ya Elimu iachwe ifanye kazi zake za awali za kutunza mtaala, shughuli ya ufundi wa vitabu na uhakiki wa machapisho yatakayotumika kwenye mfumo wa elimu ipewe chombo kingine na sekta binafsi iachiwe kwenye uchapishaji.