Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Awali ya yote nami nimshukuru Mheshimiwa Waziri na timu nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuchangia naomba nianze eneo la elimu maalum kwa maana ya ukurasa wa128, nashauri jambo moja kwa maana ya wananchi tuendelee kuhamasisha mbali na kuhamasisha kuhakikisha hatuwafichi watu hawa wenye ulemavu, tunawaandikisha ili waweze kushiriki katika nafasi ya elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la upungufu wa elimu, eneo langu la Mkoa wangu wa Katavi, hasa kwa maana ya masomo ya physics na mathematics. Tatizo la Walimu kama tulivyoongea maeneo mengine na bahati mbaya, kuna Walimu wanapangwa kuja katika maeneo yetu, lakini hawafiki. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba hilo nalo alibaini. Kuna Walimu ambao wamekuwa wakijitolea kwa muda mrefu, labda tufike mahali tuone, hawa ambao wamekuwa wakijitolea labda ajira ziende kwa watu hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoka hapo, bahati nzuri, nimshukuru Mheshimiwa Waziri, aliweza kufika Mkoa wa Katavi, aliweza kutembelea Chuo cha VETA, aliweza kutembelea shule ya watoto wa kile pale Mpanda na kwa ujumla wake, nishukuru upande wa VETA, waliwezesha fedha kwa maana ya ukarabati, lakini kuna upungufu wa takribani milioni 100 kwa maana ya awamu ile ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya ukarabati. Naomba hili Mheshimiwa Waziri alitilie maanani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, kwa maana ya eneo lile la majengo, kwa maana ya shule za sekondari, Mheshimiwa Waziri, upande wa Mpanda, shule ya wasichana, ni kweli tumeongea hapo nyuma, naomba kwa maana kama maeneo mengine nayo ile ni shule kongwe, ameiona yeye mwenyewe Mheshimiwa Waziri, tuna tatizo la uzio na ukarabati wa shule kwa ujumla wake. Najua mazingira mazuri tunapojaribu kutafuta kujua mwanafunzi anasomaje, anawezaje ku-concentrate ni pamoja na mazingira mazuri, yana nafasi yake kubwa sana katika ufaulu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka hapo, nami katika elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi, naendelea kushukuru, wakati Serikali imejipanga, kwa mfano, kwa maana ya Arusha Tech, imejipanga kwa maana ya kununua vifaa vipya. Hili naliomba sana, dunia inakwenda kwa kasi, teknolojia zinabadilika, kwa hiyo, Wizara kwa kuliona hilo, kwamba ni vizuri basi, tukaja na vifaa vipya, hili jambo naliunga mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze Wizara, kwa maana ya Mtaalam Elekezi, ule ukurasa wa 18, ambaye anakwenda kutengeneza capacity building, kwa maana ya labour market ya vitu vingine vya namna hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara ya mwisho mwaka jana, kati ya tarehe 19 na 20, nilishiriki katika mkutano mmoja mkubwa Astana, huko Kazakhstan, wenzetu, pamoja na kwamba ni nchi ambazo zimepiga hatua. Katika mkutano huo, ambao ulikuwa na kichwa cha habari Investing in Youth Living no One Behind. Watu hawa wamechambua mambo mengi, lakini katika hayo waliyochambua na hili nimeliona kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri. Nimefarijika sana kwa hilo, kwamba wenzetu ambao tayari wamekwishaendelea, lakini wameona kwamba namna pekee ya kufanya, ni kufanya katika sura ifuatayo:-

Kwanza, ni kuamsha ufahamu kuhusu elimu, afya, ajira na masuala ya kijamii, lakini ufahamu huu, especially kwa those ambao ni disadvantaged. Tukitoka hapo, wameamua kwenda na jambo moja, uwezeshaji zaidi, elimu bora, kwa maana ya vocational training, inayokwenda na ushindani na mahitaji ya soko la ajira, uchumi wa dunia na maendeleo ya teknolojia. Haya yote ambayo wajumbe wamekuwa wakiongea, kama hatuendi kuangalia mahitaji ya soko, uchumi wa dunia, mabadiliko ya teknolojia, tutaendelea kupiga kelele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo kama halitoshi, kuna suala, wenzetu wamekuja na kitu wanasema, review and adjust the education system and vocational training in line with economic, social and entrepreneur realities. Kwa hiyo, haya yote nilikuwa nasema, wenzetu huko duniani wameendelea kuaona kwa sura hiyo. Kwa hiyo, niombe, katika mazingira haya, ambapo nilijaribu kusoma kitabu cha Mheshimiwa Waziri, bahati nzuri, nilipokuwa nikitoka ukurasa mmoja nafikiria kwamba jambo hili linalogusa kuwawezesha watu kwa sayansi na teknolojia sasa hivi linapatikana wapi, nalikuta ukurasa wa pili, nikitoka ukurasa wa pili nalikuta ukurasa wa tatu. Kwa hiyo, katika hilo niendelee kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, kwa kuheshimu muda, naunga mkono hoja. (Makofi)