Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza kabisa, napenda kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri lakini pia napenda kuipongeza Serikali kwa ujenzi wa maktaba mpya na ya kisasa. Maktaba hiyo ndiyo kubwa kwa East Africa nzima. Maktaba hiyo inakwenda sasa kuwapata watafiti wetu nguvu na ufanisi wa kuweza kufanya tafiti zao vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maktaba hiyo pia inakwenda kuwaisaidia wanafunzi wa elimu ya juu nchi nzima kuweza kufikia yale mahitaji ambayo yalikuwa yanatakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vie muda wangu mchache, naomba sasa niende moja kwa moja kwenye mchango wangu. Suala la kwanza ambalo nitaliongelea ni Sera ya Elimu versus Sera ya Uchumi wa nchi. Nchi zote duniani, Sera ya Elimu ndiyo inatoa dira na mwelekeo wa Sera ya Uchumi wa nchi. Kama tunavyofahamu, Wizara ya Elimu ndiyo mdau na ndiyo yenye dhamana ya kuleta rasilimali watu ambao wataweza sasa kujenga uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda na uchumi huu kwa kiasi kikubwa sana unahitaji rasilimali watu, wenye elimu na ujuzi wa level ya kati, sio level ya juu. Kama tutakubaliana na hilo, niiombe sasa Serikali yangu, nafahamu inasikia na ina lengo la kui-support hii Sera ya uchumi, iende sasa ikaboreshe mitaala katika vyuo vyetu vya stadi za kazi, iende ikaboreshe mitaala na ufanisi katika vyuo vyetu vya VETA. Kwa sababu hizo ndiyo taasisi ambazo zitatuletea nguvukazi ya vijana na watu ambao wataendesha viwanda vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuongea hayo, naomba sasa kidogo niende nikagusie masuala ya watu wenye mahitaji maalum hasa wale wenzetu ambao wana shida ya kusikia au kwa lugha rahisi, viziwi. Hawa watu wenye kundi maalum hili wanakutwa na changamoto kubwa. Changamoto kubwa ni kwa sababu hawana uwezo wa kufanya mawasiliano ya moja kwa moja na watu wa kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto hii inasababisha hata ufanisi wao katika masuala ya elimu wakiwa shuleni unakuwa mgumu sana kiasi kwamba huwa wanakosa msaada kwa wenzao. Rai yangu kwenye hili, napenda kuishauri Serikali ione sasa umuhimu wa kuanzisha elimu ya lugha ya alama iwe kama somo katika shule zetu ili sasa hawa wenzetu waweze kufaidika na mfumo wa elimu wa nchi yetu.

Mheshimiwa Menyekiti, katika kufanya hili, hatuendi tu kuwasaidia watu ambao hawana uwezo wa kusikia kwa vile soko la ajira kwa wakalimani sasa hivi ndani na nje ya nchi liko very hot. Tunakwenda ku-create ajira kwa vijana ambao sasa watakuwa wamepatiwa elimu ya lugha ya alama kwa maana ya kwamba tutapata wakalimani ambao watapata ajira ndani na nje ya nchi yetu. Kundi hili lina changamoto nyingi sana. Hiyo ya kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee ya pili. Kati ya vyuo ambavyo tunavyo nchini, ni vyuo vinne tu ndiyo ambavyo mpaka sasa vina wakalimani, kiasi kwamba kuna wanafunzi ambao wanafanikiwa kufika mpaka ngazi ya shahada, wanafika vyuoni na huwa wanakosa misaada ya kuweza kuendelea au ku-cope kwa sababu hawana vyuo husika au hawana vyuo maalum kwamba hawa vyuo vyao specifically ni hivi. Huwa tunawachanganya pamoja na wanafunzi wengine na wakifika kule wanakosa wakalimani wa kuweza kuwasaidia kuweza ku-cope na masomo.

Mheshimiwa Waziri, naomba hili ulichukue. Tuna watu wenye ulemavu wa kusikia ambao ni very genius, wanahitaji msaada mdogo tu wa wakalimani ili na wao sasa waweze ku-cope vizuri na masomo wakiwa vyuoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto nyingine kwa hawa wenzetu ni suala zima la ajira. Kila anayesoma ndoto yake ni kuweza kutumia elimu yake kumfikisha au kuweza kutumia elimu yake kumkwamua kwenye masuala ya kiuchumi, lakini kwa bahati mbaya sana bado Serikali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda wako umekwisha.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Eh!

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.