Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa namna ya pekee, naomba nipongeze uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga ukiongozwa na DC mahiri, mchapakazi, Ngolo Malenya kwa utaratibu wake wa kuweka mikakati na kutekeleza kwa ajili ya kuinua elimu ya Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kule vyombo vya habari hakuna Lakini vyombo vya habari vingekuwepo tungeenda sambamba na watu wengine, lakini mimi nitazifikisha habari za Ulanga katika Bunge hili ili mjifunze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Ulanga tumeweka lunch program kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari. Wanafunzi wanaenda wanakula chakula huko huko wanapata muda wa kutosha wa kujisomea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna kambi kwa ajili ya wanafunzi wale wanaojiandaa kufanya mtihani. Sasa hivi tuna kusanya vyakula kwa ajili ya kupeleka katika shule ambazo watafanya mtihani kidato cha sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tumebuni miradi kwa ajili ya kuinua vipato vya walimu. Tumewapa mashamba, yaani mwalimu akienda kule inaitwa “gusa unite.” Akikaa huko, hawezi kuondoka tena. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeunganisha wadau wa elimu, tumepata zaidi ya shilingi milioni 150 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa. Tumebuni utaratibu wa kufanya mabonanza kwa ajili ya kuwapa motisha wale walimu ambao wanafundisha katika mazingira magumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Ulanga kuna maeneo hayafikiki kwa baiskeli, hakuna mawasiliano wala umeme. Kwa hiyo, tumeweka motisha kwa ajili ya kuwasaidia walimu kama hao wapate moyo kwa ajili ya kufundisha. Ndiyo maana Mheshimiwa Waziri katika maombi yetu tumeomba tuwekewe VETA ili kuwaunga mkono Ulanga kwa jitihada zote za kuinua elimu hizi wanazozifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Profesa Ndalichako. Unajua Profesa Ndalichako yuko tofauti na Maprofesa wengine, Profesa wa CCM, Profesa ambaye yuko updated kama iPhone. Naomba nimpongeze yeye pamoja na Naibu Waziri, pamoja na Katibu Mkuu wake Akwilapa pamoja na AveMaria. Wamekuwa wasikivu, wamekuwa wakiweka mikakati mizuri na kuitekeleza kwa ajili ya kuboresha elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukilalam ika mwanzo lakini amekuwa akitusikiliza na kuyafanyia kazi. Ila kuna kazi kidogo naomba akae vizuri na watu wa private schools ili aweze kwenda sawa kwa sababu TAMISEMI wamekuwa kama kivuruge; wanataka kusimamia shule za private na hao hao wamekuwa wanamiliki shule za Serikali. Sasa huyu referee mchezaji amekuwa anaharibu mambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko kodi nyingi sana na ziko ambazo zimetolewa lakini bado wanachokonoa private kwa chini kwa ajili ya kuwadai hizo kodi. Kwa mfano, kila mwanafunzi mmoja anatakiwa alipe fire shilingi 20,000/=. Huu ni wizi mkubwa ambao Serikali inafanya kwa shule za private. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa elimu bure. Walioongea hapa wanasema elimu bure imefanywa kwa mustakabali wa siasa. Ndiyo nakubali, si iko kwenye Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi. Sasa nataka wakawaambie waliowaambia elimu bure imefanywa kwa ajili ya siasa. Ulanga kwa mwaka huu wa fedha ambao unaisha, tumepata gari moja kwa ajili ya ukaguzi wa elimu. Ulanga tumepata pikipiki 19, wale waratibu wa elimu zamani walikuwa wanatembea kwa mguu, sasa hivi kila mratibu wa elimu ana pikipiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata shilingi milioni 214 kwa ajili ya kumalizia maboma ambayo wananchi walianza kujenga. Tumepata zaidi ya shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni na madarasa katika shule mbalimbali. Naipongeza Serikali kwa kutoa ajira kwa walimu 4,000 Ulanga; na yenyewe tumepata japokuwa kidogo. Naiomba Serikali iongeze jitihada ya kuajiri walimu kwa sababu mtaani wako wengi, kuna walimu zaidi ya 100,000. Kwa hiyo, Serikali iongeze ajira kwa walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ulanga tunazalisha wanafunzi wa form four 1,000 - 1,200 kwa mwaka. Wanaokwenda kidato cha tano na cha sita hawazidi 200. Wanabaki 1,000; hao 1,000 tunawapeleka wapi? Ndiyo maana nimekuomba Mheshimiwa Waziri, tusogezee VETA, eneo tayari tunalo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kukarabati shule kongwe lakini kwangu mmeisahau shule moja inaitwa Kwiro. Kwiro ni shule ya zamani wamesoma vigogo wakubwa, nikiwemo mimi. Kwa hiyo, naomba muikarabati hiyo shule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kuongeza fungu la Bodi ya Mikopo kufika shilingi bilioni 423, lakini changamoto imekuwa kubwa kwa sababu wanafunzi ni wengi. Serikali imeshindwa kuchanganua kupata wanafunzi masikini halisi na wanafunzi wenye kipato cha juu. Kwa hiyo, tatizo limekuwa kubwa. Pia makato ya Bodi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)