Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru ningependa kumuomba Mheshimiwa Waziri, matokeo ya mitihani ya kidato cha nne form four na form six kwa Visiwani hasa Unguja na Pemba kuendelea kila wakati kuwa siyo mazuri kulingana na takwimu ambazo zinatokea, hivi wewe halikukeri hili? Pia una mkakati gani hasa wa zaida kuona kwamba matokeo kutoka Visiwani, Unguja na Pemba kwenye mikoa yote sasa yanabadilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vifaa vya sayansi shule za sekondari (O’level) kuna upungufu mkubwa sasa wewe na mwenzako Wizara ya Elimu Zanzibar mna mkakati gani wa ziada? Leo yaani mitaala inabadilika inachukua muda mrefu kufika kule Zanzibar, sasa kuna tatizo gani la ziada ambalo linaonekana hili kuna upungufu kama huu na bado naona tu na matokeo ya Zanzibar kila siku yanaendelea kuwa mabaya hili jambo mkae mlione.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la kusikitisha sana, kuna kwenye NECTA Baraza la Mitihani wewe ndio ulikuwepo Mheshimiwa mwenyewe huko, lakini uwiano wetu washiriki waliotoka Zanzibar ni wa aina gani kiasi ambacho kwamba Zanzibari kule wapo na washiriki wao na jinsi gani ya kushirikishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mlisema matokeo mabaya Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Kusini Unguja, Kaskazini Unguja, Mjini Magharibi, lakini wewe ulikuwepo jikoni. NECTA je, Zanzibar iko kiasi gani mtuambie na sisi tunapata uchungu kweli kuona Zanzibar bado hatupati matokeo mazuri kumbe kuna mambo ambayo yanahitaji yatelekezwe. Ningeomba sana Mheshimiwa Waziri utupe mpango makakati baina yako na mdau mwenzako wa Zanzibar kuona kwamba matokeo hasa ya form four na form six kwa upande wa Visiwani Unguja na Pemba yaani Zanzibar yanakuwa mazuri, hilo lilikuwa la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili suala la fedha za maendeleo kuhusu wahisani. Tumesema muda mrefu sana kwamba hatuwezi kupata maendeleo ya kweli kama tunategemea wahisani hawa wafadhili. Ukingalia katika maeneo mbalimbali kuna kuimarisha ubora wa elimu ya sekondari 4590 item kwenye Sub Vote 2001, bilioni 30.8 zote za wahisani. Kwenye Idara ya Udhibiti bora vilevile, nako kuna bilioni 16 Education Program for Result, fedha za wahisani. Kwenye elimu, Idara ya Elimu ya ualimu nako vilevile, Teachers Education Support Program billion 15.4, zote ni wahisani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa bajeti yote ya maendeleo imeenda kwenye wahisani, wahisani, wahisani hawa ambao hawaleti fedha, nawashangaa na ndiyo maana tukasema leo tutumie vitabu hivi na wale wenzangu waliosema kwamba hata kwenye fedha za maendeleo ambazo za mikopo zimeenda kule. Kwa hiyo kuna Volume II, kuna Volume IV, kuna Randama hapa, juzi tulipokuwa tunatumia vitabu hapa wengine wanasema tutavua nguo, tutavua nguo, alisema Waziri mmoja hapa na kama leo angekuwepo Waziri Kangi leo ningemwambia vua nguo kwa sababu sisi tunatumia vitabu, vua kweupe mchana kweupe hapa. Haiwezekani tunataka maendeleo ya kweli ikawa tunatenga asilimia zaidi ya 60 kwa wahisani, haiwezekani hata kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye higher education, elimu ya juu Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu na uko makini kweli leo. Nenda kwenye 2228 nako ni vilevile, kuna Support on Research and Development. Tunakwenda kufanya utafiti kutuwezesha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Ardhi, MUHAS kufanya utafiti kwa maendeleo ya elimu. Bilioni 10.4 kitabu cha Volume IV, mmedharau Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mmedharau MUHAS, mmedharau Chuo Kikuu cha Ardhi mmedharau, fedha hizi za wahisani yaani kila kitu wahisani, wahisani, hawa tunawaita mabeberu nawashangaa kweli kweli. Hakuna kitu ambacho kinakera kwamba fedha … (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante, mengine utaandika.

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Atakayevua nguo na avue! (Kicheko/Makofi)