Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, katika Wilaya ya Missenyi, Kata ya Kakunyu nimepokea malalamiko mengi ya baadhi ya watu kupewa PI - Persona non grata na kutakiwa kuondoka ndani ya saa 24.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri anipatie orodha ya majina ya Utaifa wa watu waliokuwa wanakaa Kata ya Kakunyu na wakapewa ‘PI’. Katika mikutano yangu ya hadhara katika Kata ya Kakunyu nilipokea malalamiko mengi, pia ya baadhi ya wananchi kukamatwa usiku nyumbani kwao na kupigwa viboko na kulazimishwa wakubali kwamba wao si Watanzania. Naomba Mheshimiwa Waziri afafanue kama vitendo vya kukamatwa watu usiku na kuwapiga viboko ndiyo utaratibu mpya wa kuwatambua Watanzania na wasiokuwa Watanzania hasa katika Kata ya Kakunyu, Wilayani Misenyi.