Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Spika, nampa hongera Mheshimiwa Waziri Kangi Lugola kwa majukumu. Nachukua fursa hii kukumbusha juu ya wito wa Serikali kwa wananchi kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Tarafa ya Chipanga, Wilayani Bahi waliamua kujenga Kituo cha Polisi cha Tarafa toka mwaka 2003 na kukikamilisha lakini hadi sasa hakijafunguliwa takribani miaka 16 sasa. Wananchi walichangia zaidi ya milioni 40 wakati huo, lakini wamekatishwa tamaa na Jeshi kutokukipokea kituo hicho na kukifungua. Kituo hicho kina umuhimu mkubwa kikifunguliwa kwa kulinda usalama wa mali na wananchi. Naomba sasa kifunguliwe. Ahsante.