Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, posho za wazee wa Mahakama; Babati hawajawahi lipwa miaka miwili iliyopita, wazee wamehangaika bila mafanikio. Sasa naomba kufahamu wazee hawa wamehangaika sana watalipwa lini?

Mheshimiwa Spika, fidia ya wananchi ambao maeneo yao yalichukuliwa na jengo lao la Mahakama, Mkoa wa Manyara na Mahakama ya Wilaya ya Babati pale Mtaa wa Negamsii, Kata ya Bagara, Jimbo la Babati Mjini tangu 2004 hadi leo wananchi hawajalipwa fidia japo Mahakama imeshajenga majengo yao na wananchi hawajalipwa. Naomba kufahamu Mahakama kama chombo cha haki ni kwa nini imewanyima wananchi fidia yao na lini watalipwa?