Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ya kuchangia. Niliuliza swali kuhusu kutokuwepo kwa gereza lenye sifa ya kuwa gereza katika Wilaya ya Igunga. Gereza la Igunga halina ngome, hakuna gereza la wanawake na hulazimika kupeleka wafungwa wa kike kwenye Gereza la Wilaya ya Nzega. Gereza hilo pia halina nyumba za askari na halina ofisi za utawala. Kutokana na hali hiyo tunaiomba Serikali itafute fedha za kufanya mambo yafuatayo:-

(a) Ujenzi wa ngome;

(b) Ujenzi wa jengo la utawala;

(c) Ujenzi wa gereza la akinamama; na

(d) Ujenzi wa nyumba za askari.

Mheshimiwa Spika, sasa tumeanza kuwahamasisha wananchi na viongozi wa wilaya kuchangia ujenzi wa ofisi za utawala na nyumba za askari. Tunaomba sana Serikali ituunge mkono kwenye suala hili ili kuondoa adha wanayopata wafungwa na mahabusu katika Wilaya ya Igunga. Wilaya ya Igunga pia haina vitendea kazi kama magari na computer kwa ajli ya Jeshi la Polisi na hii inasababisha uduni wa huduma inayotolewa na Jeshi la Polisi. Wilaya ya Igunga ina vituo vya polisi katika Tarafa ya Manonga-Chome, Tarafa ya Simbo Simbo; Tarafa ya Igurubi, Igurubi; Tarafa ya Igunga, Igunga na Kituo cha Kata ya Nanga. Vituo vyote hivi vinahudumiwa na gari moja ambalo lipo katika Kituo cha Wilaya ya Igunga. Tunaomba Serikali inunue magari kwa ajili ya Vituo vyote vya Polisi katika Wilaya ya Igunga.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa viongozi wa Wilaya akiwemo DC, Mbunge, DED na wengine tumeanza mchakato wa kujenga Vituo vya Polisi vya Kata za Igunga (Mwanzugi) na Lugubu ili kukabiliana na ongezeko la watu katika maeneo hayo. Tunaomba Serikali ituunge mkono. Ahsante sana.