Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mambo ya Ndani ni Wizara muhimu sana katika usalama wa raia na mali zao. Wizara hii inatakiwa Serikali kuwa na mikakati thabiti ya kutoa mafunzo kwa vijana wetu Askari ili kuwa imara kila wakati, kuboresha mazingira yao kwa kuwajengea nyumba, kupewa usafiri kama pikipiki, nyumba zao kuwekewa umeme, maji na kulipwa posho na kuongezewa mishahara yao. Pia kupandishwa vyeo kwa Askari hasa kitengo cha Polisi, Uhamiaji na Magereza, vyeo vyao vinachelewa sana, namaanisha kuwapandisha vyeo Askari wanaostahili kupandishwa. Naipongeza Serikali kwa kuwajengea nyumba Askari wa Uhamiaji wa hapa Dodoma. Hili ni jambo zuri sana kwa kuwajali Askari wetu.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.