Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kuipongeza Serikali inayoongozwa na Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Waziri wake Mheshimiwa Kangi Lugola kwa ufanisi wake.

Mheshimiwa Spika, hali za Magereza yetu nchini ni mbaya, lazima kuwe na mkakati wa kufanya ili kunusuru hali hii. Ndani ya Magereza kuna wafungwa wenye vipaji vyao ambao wanaweza kutumika kama sehemu ya uzalishaji na sehemu ya kipato. Mfano, kuna wafungwa wenye taaluma ya carpenter (utengenezaji wa furniture), wengine ni wajenzi. Hao hao wangetumika kwenye matengenezo ya furniture za Magerezani au hata ujenzi wa ndani lakini pia furniture zingeuzwa kwenye Taasisi za Serikali ili waweze kupata mapato. Hii ingesaidia sana kuongeza hela ya bajeti mnayoomba, ingesaidia kwenye matatizo mengine kama kununua vitendea kazi kwa ajili ya wale wenye vipaji vya kuzalisha.

Mheshimiwa Spika, hii ingetumika kwa taasisi zote kwa kuwa hata Polisi wapo wenye vipaji vya ujenzi, wawezeshwe kwa kupatiwa vifaa. Hizi nyumba tunazolalamika wanaweza kuzijenga wenyewe kwa kiwango kizuri. Tutumie sana vipaji vyao kuzalisha na kuingiza vipato. Ni aibu mtu anasimama hapa anaombea Askari mafuta. Tubadilike, hizi hela zinazopatikana zipelekwe kwenye maeneo ya uzalishaji na kujiwekea mazingira mazuri.

Mheshimiwa Spika, tuzipe hizi taasisi uhuru wa kuonesha vipaji vyao katika maendeleo na kujiweka wenyewe katika mazingira mazuri. Tuachane na mawazo ya kunufaisha watu wengine kwa kutumia neno tenda. Taasisi hizi zina uwezo wa kufanya vitu wenyewe na kuleta tija, tuwape nafasi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.