Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uhai na uzima. Naomba Askari wetu waongezewe mishahara katika bajeti hii kwani wanafanya kazi katika mazingira magumu sana, usiku na mchana, jua lao mvua yao. Kwa hiyo, naishauri Serikali iwaangalie Askari wetu hawa waongezewe posho kwani hali ya maisha ni ngumu sana. Posho ya shilingi 300,000/= kwa mwezi ni ndogo sana, haitoshi. Ina maana Askari huyu pamoja na familia yake inabidi atumie shilingi 10,000/= kwa siku kuanzia asubuhi mpaka jioni. Je, itamtosha Askari huyu? Hali hii inasababisha Askari wetu wajihusishe na masuala ya rushwa ili wakidhi mahitaji yao.

Mheshimiwa Spika, nyumba wanazoishi Askari wa Magereza ni aibu, nyumba za Polisi Mtwara ni za tangu enzi za mkoloni na hazijaboreshwa. Jengo la Kituo cha Polisi cha Mtwara ni chakavu, kuta zina nyufa, hali inayosababisha kuwa na hatari kwa Askari wetu na wanaweza kuangukiwa na jengo hilo.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, tunaomba Jeshi la Polisi lisitumike vibaya kwenye masuala ya kisiasa. Jeshi hili lifanye kazi yao kwa weledi bila kuegemea upande wowote.