Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu wake pamoja na Katibu Mkuu kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya. Wana Namtumbo wanafurahia utendaji wao na wanaomba yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, wanachi wa Namtumbo wanaomba wapewe Vitambulisho vya Taifa, maana taarifa zao na picha vimechukuliwa muda mrefu sana lakini hawaoni matokeo.

Mheshimiwa Spika, lingine, baadhi ya Askari Polisi wasio waaminifu wanaodai hawajalipwa haki zao wanawanyanyasa wakazi wa Namtumbo kwa kuwabambikizia kesi na kwa waendesha bodaboda kushikwa mara kwa mara na kutakiwa walipe faini bila kosa lolote. Mtusaidie tuishi kwa amani bila bugudha ya baadhi ya Maaskari wasio waaminifu.

Mheshimiwa Spika, Polisi wanatumika vibaya na WMA ya Mbarang’andu na Kimbanda kwa kuwanyanyasa wakazi wa Namtumbo wanaoishi karibu na maeneo ya Hifadhi za Jamii (WMA) kwa kuwapa adhabu za kuwatweza utu wao na kutakiwa kulipa faini ama tozo za malaki na mamilioni ya shilingi eti kwa sababu wamekutwa majumbani mwao wamepika samaki au uyoga wakidai lazima watakuwa wameingia kwenye maeneo ya Hifadhi za Jamii kinyume na Sheria.

Mheshimiwa Spika, nashauri Polisi wasitumike kwa operesheni za aina hii, badala yake hizo WMA zijisimamie zenyewe. Polisi walipwe stahiki zao kwa wakati ili wasirubuniwe na viongozi wa WMA wanaowalipa posho zinazotoka kwa NGO za Kimataifa ambazo zina dhamira mbaya za kuwagombanisha wananchi na Serikali yao inayoongozwa na mpendwa wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.